Nchi zakumbushwa kuanzisha vituo vya taarifa na udhibiti wa sumu
: Sumu ni tatizo la afya ya umma lakini bado nchi zinapuuza kuweka vituo vya kudhibiti
Duniani kote tatizo la binadamu kukumbwa na sumu halipatiwi kipaumbele au hata haliripotiwi kuwa ni tatizo la afya la umma. Llicha ya kwamba shirika la Umoja wa Mataifa la afya ulimwenguni, WHO linapendekeza kila nchi kuwa na vituo vya kufuatilia na kutibu bado ni chini ya nusu ya wanachama 194 wa shirika hilo wana vituo hivyo na miongoni mwao ni Thailand.