Syria: pande kinzani zimeshindwa kutimiza sheria za kimataifa kuhusu kushambulia hospitali
Pande kinzani katika vita vya Syria ambavyo vimeingia mwaka wa kumi sasa zimeshindwa kutimiza wajibu wao chini ya sharia za kimataifa wa kuepuka kushambulia hospitali na vituo vingine vya raia ambavyo vimeorodheshwa katika orodha ya Umoja wa Mataifa amesema leo Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres.