Skip to main content

Chuja:

Radio ya Umoja wa Mataifa

Mwanza Youth reporter

Wasichana shirikini michezo kwa kucheza na kutangaza

Radio, michezo na jinsia ni mada ambayo imechambuliwa kwa kina na vijana wa mtandao wa wanahabari vijana kutoka Mwanza nchini Tanzania. Uchambuzi huo umeendana na maudhui ya siku ya redio duniani hii leo ya Radio na Michezo. Katika makala hii, mwanahabari kijana Rashid Malekela anazungumza na vijana wenzake wa kike na wa kiume kufahamu ni kwa jinsi gani mada hizo zinaoana na zaidi ya hapo zinasaidiaje kubeba jukumu kubwa la radio la kuliemisha, kuhabarisha na kuburudisha.

Sauti
4'5"

Muziki waeneza amani Somalia

Kwa zaidi ya miongo miwili sasa, Somalia imeghubikwa na migogoro ikiwemo mashambulizi ya Al-Shabaab na mapigano ya wenyewe kwa wenyewe, na hivyo kusababisha maelfu ya raia  kupoteza maisha, makazi na wengine kusaka hifadhi nchi jirani. Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa usaidizi nchini humo, UNSOM, kwa kushirikiana na serikali unatumia njia mbalimabli kuhakikisha mkataba wa amani umetekelezwa ili  watu waweze kurejea makwao. Je ni mbinu gani zinatumika kuchagiza amani? Joshua Mmali anaangazia kupitia makala hii.

Makombora yetu "hayakiuki" kanuni zozote- Korea Kaskazini

Hoja ya Korea Kaskazini kuendelea kufanya majaribio ya nyuklia kinyume na makubaliano ya kimataifa imejadiliwa kwa kina leo kwenye Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, wakikutana mawaziri wa mambo ya nje na mabalozi ambao nchi zao ni wajumbe wa baraza hilo.

Korea Kaskazini na Korea Kusini zilihudhuria kwa mujibu wa kanuni namba 37 ya Baraza la Usalama ambapo Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres akasisitiza umoja ndani  ya chombo hicho ili hatihati ya usalama iliyopo isiongezeke.