Guterres ataja mambo matatu ili kuimarisha ulinzi wa raia kwenye mizozo
Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa leo limekuwa na mjadala wa wazi kuhusu ulinzi wa raia kwenye mizozo ambapo Katibu Mkuu Antonio Guterres amesema kadri giza linavyozidi kutanda katika ulinzi wa raia kwenye mizozo, ni lazima kuweka na kutekeleza kanuni za kuimarisha ulinzi.