Skip to main content

Chuja:

Qu Dongyu

UNDP/Pierre Michel Jean

Ripoti ya FAO yaonesha mchango wa uvuvi na ufugaji wa samaki katika kuimarisha uhakika wa upatikanaji wa chakula

Mkutano wa Umoja wa Mataifa kuhusu bahari ukiwa katika siku ya tatu hii leo huko Lisbon nchini Ureno Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo FAO limesema ongezeko kubwa la ufugaji wa samaki sambamba na uvuvi wa kimataifa umesababisha mazao ya vyakula vya majini kuwa kwenye rekodi ya juu katika kuchangia kwa kiasi uhakika wa chakula na lishe katika karne hii ya Ishirini na moja.

Taarifa ya Leah Mushi.

Sauti
2'26"
Lori linapakua nafaka katika kiwanda cha kusindika nafaka nchini UkrainE.
© FAO/Genya Savilov

G7: FAO yatoa mapendekezo ya kukabiliana na uhaba wa chakula wa sasa na ujao

Mkurugenzi Mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo FAO Qu Dongyu ametoa wito kwa nchi tajiri zaidi duniani G7 kusaidia kukabiliana na uhaba wa chakula katika siku zijazo kwani vita inayoendelea nchini Ukraine imepunguza usambazaji na kupandisha bei juu katika viwango vya kuvunja rekodi na kuyaweka mashakani mataifa ambayo tayari yana hatari ya kuathirika kote barani Afrika na Asia.

FAO Tanzania

FAO yajivunia ushirikishaji vijana kwenye kilimo

Mkurugenzi Mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la chakula na kilimo, FAO Qu Dongyu ametoa ujumbe wake kwa mwaka mpya wa 2022 huku akitaja mafanikio ambayo shirika hilo limefanikisha mwaka huu wa 2021 licha ya changamoto ya janga la ugonjwa wa Corona au COVID-19.
Katika salamu hizo kwa njia ya video Bwana Qu amesema mafanikio hayo ni pamoja na mikutano waliyoendesha ili kufanya kazi usiku na mchana kuleta mabadiliko yanayoweza kuondoa njaa duniani.

Sauti
1'47"
Mkakati wa FAO wa kusaidia kukabiliana na njaa kwenye bonde la Ziwa Chad umeleta nuru kwenye uhakika wa chakula.
FAO/Pius Utomi Ekpei

‘Mkono kwa mkono’ kunusuru njaa katika nchi maskini- FAO

Shirika la chakula na kilimo duniani, FAO limesema kitendo cha nchi wanachama wa Umoja waMataifa kusaidia na kuunga mkono harakati za shirika hilo kama mpango mpya wa Mkono kwa Mkono,  kitaasaidia kuchagiza mafanikio ya malengo ya maendeleo endelevu, SDGs hususan lile la kutokomeza njaa, na hivyo kutomwacha nyuma mtu yeyote.