Chuja:

punguzo

Ushirikiano baina ya nchi za Asia ya Kati na Afghanistan ni dhahiri- Guterres

Umoja wa Mataifa umesema uko tayari kusaidia nchi za Asia ya Kati zinapoimarisha ushirikiano baina yao na Afghanistan ili kufanikisha malengo ya amani, maendeleo endelevu, utulivu na usalama.

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António  Guterres amesema hayo leo wakati akihutubia mkutano wa Baraza la Usalama uliokutana kujadili ubia wa kikanda kati ya Afghanistan na Asia ya Kati.

Bwana Guterres ametolea mfano ushirikiano wa kielimu uliopo sasa kati ya Kazakhstan na Afghanistan..

(Sauti ya António  Guterres)

UN yapunguza bajeti yake

Bajeti ya umoja wa Mataifa kwa mwaka 2018-2019 yenye kurasa zaidi ya elfu 8 zilizosheheni maelezo ya mipango mbalimbali na takwimu za taasisi hii kubwa zaidi duniani ilipitishwa mwishoni mwa juma na nchi 193 wanachama wa Umoja huo ikiwa na upungufu wa mamilioni ya dola ikilinganishwa na mwaka 2016-2017 unaomalizika. Tuungane na Assumpta Massoi anayetudadavulia zaidi kuhusu kilichomo, kilichoathirika zaidi na matarajio ya baadaye katika kuhakikisha Umoja wa Mataifa unafanya kazi kwa ufanisi na unawajibika kwa nchi wanachama na walipa kodi.