Uwekezaji zaidi wahitajika ili kukabiliana na njaa- FAO
Ongezeko la idadi ya watu wenye njaa duniani ni kiashiria kuwa mbinu mpya zahijitaka ili kubadili mwelekeo huo.
Mkurugenzi Mkuu wa shirika la chakula na kilimo duniani, FAO José Graziano da Silva amesema hayo akihutubia kikao cha baraza la shirika hilo mjini Roma, Italia.
Amenukuu takwimu za hivi karibuni zinazoonyesha kuwa idadi ya watu wenye njaa ni milioni 815, ikiwa ni ongezeko la kwanza katika kipindi cha zaid ya muongo mmoja.