Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

PPR

Sehemu ya madhara ya kimbunga Idai katika eneo la bandari ya Beira nchini Msumbiji.
WFP/Maktaba

IAEA yaisaidia Msumbiji kukabiliana na maradhi ya mifugo baada ya mafuriko:

Shirika la kimataifa la nguvu za atomiki IAEA, limepeleka vifaa vya dharura ili kuisaidia Msumbiji kupambana na mgonjwa ya mifugo kama homa ya Afrika ya nguruwe, ugonjwa wa miguu na midomo  au homa ya bonde la ufa magonjwa ambayo yanaweza kuleta athari kubwa na kutishia mustakabali wa mifugo na binadamu baada ya mafuriko yaliyosababishwa na vimbunga vya hivi karibuni.

Nchini Niger kondoo zinakabiliwa na hatari ya ugonjwa wa PPR
©FAO/Andrew Esiebo

Ugonjwa wa PPR waua mamilioni ya kondoo, mbuzi na maisha ya wafugaji

Zaidi ya nchi 45 leo zimesisitiza ahadi yao ya kutokomeza ugonjwa wa PPR au tauni inayokatili Wanyama wengi wadogo kama mbuzi na kondoo ifikapo mwaka 2030. Kwamujibu wa shirika la chakula na kilimo FAO na lile la kimataifa la afya ya mifugo OIE, wakizungumza katika mkutano uliomalizika leo mjini Roma Italia, ugonjwa huo wa kuambukiza unaua mamilioni ya mbuzi na kondoo kila mwaka .