Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

POLAND

25 SEPTEMBA 2023

Hii leo jaridani tunaangazia machafuko nchini Ukraine na mkutano wa kimataifa huko Rome kuhusu marekebisho ya mfumo wa ufugaji wa wanyama. Makala tunasalia hapa makao makuu ya Umoja wa Mataifa na mashinani tunakupeleka nchini Poland, kulikoni?

Sauti
12'56"
© Unsplash/Jose Chinchilla

Harakati za Benki ya Dunia kuuboresha mji wa Libiąż, Poland dhidi ya makaa ya mawe

Kuondoa makaa ya mawe ni mojawapo ya hatua muhimu zaidi za kupambana na mabadiliko ya tabianchi na kulinda sayari. Kuhama kutoka katika matumizi ya makaa ya mawe hadi nishati safi hupatia jamii fursa muhimu za kiuchumi na kijamii pia. Mji wa Libiąż, Poland, ulio katika eneo la uchimbaji wa makaa ya mawe ambao umedumu kwa karne nyingi, uko katikati ya mabadiliko haya.

Sauti
3'27"

25 NOVENBA 2022

Hii leo jarida linaangazia afya nchini Haiti na ujenzi wa amani hasa kwa lengo la kuepusha vijana kutumbukizwa kwenye vikundi vyenye msimamo mkali huko Garissa nchini Kenya. Makala tunakwenda nchini Poland na Mashinani nchini Ethiopia, kuliko ni?  

Sauti
10'28"
Bibi akmhudumia mjukuu wake kwenye hospitali ya watoto mjini Kyiv nchini Ukraine
© UNICEF/Oleksander Ratushniak

Vita Ukraine yasababisha uhaba wa Oksijeni itumikayo kutibu wagonjwa - WHO

Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa hii leo tena limekutana kujadili vitisho vya amani na usalama duniani ikijikita zaidi katika uvamizi wa Urusi nchini Ukraine ambapo Mkuu wa Idara ya siasa kwenye Umoja wa Mataifa Rosemary DiCarlo amesema dalili nzuri zilizoonekana wiki hii kufuatia mazungumzo kati ya wawakilishi wa mataifa hayo mawili bado hazijazaa matunda yoyote.