Afisa wa UN asema mara ya kwanza ndege nyingi zisizo na rubani kupenya kwa kina kwenye anga la nchi jirani
Alasiri ya Ijumaa Septemba 12, 2025, Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limekutana kwenye kikao cha dharura kilichoitishwa na Poland kuhusu ndege zisizo na rubani za Urusi zilizorushwa na taifa hilo la Ulaya Mashariki kuelekea maeneo ya Belarus na hatimaye kuingia anga la Poland usiku wa kuamkia leo.