Guterres: Ikiwa dunia inataka kupambana na mabadiliko ya tabianchi, njia ni kuhamia katika nishati jadidifu
Mkutano Mkuu wa 13 wa Shirika la kimataifa la nishati jadidifu, IRENA umeanza rasmi hii leo huko Abu Dhabi nchini Falme za Kiarabu UAE ambapo umewaleta pamoja wakuu wa nchi, Mawaziri na watoa maamuzi wa masuala ya nishati kutoka mashirika ya kimataifa, wadau wa kimataifa na wahusika binafsi lengo likiwa ni kutathmini maendeleo na kuainisha ajenda za utekelezaji ili kuharakisha mchakato wa dunia kuhamia katika matumizi ya nishati jadiifu.