Skip to main content

Chuja:

PGA

Modera inanufaika kutoka kwa kiwanda cha nguvu cha Megawati 6 kilichowekwa katika kijiji cha karibu cha Sujjanpura.
UN News

Guterres: Ikiwa dunia inataka kupambana na mabadiliko ya tabianchi, njia ni kuhamia katika nishati jadidifu

Mkutano Mkuu wa 13 wa Shirika la kimataifa la nishati jadidifu, IRENA umeanza rasmi hii leo huko Abu Dhabi nchini Falme za Kiarabu UAE ambapo umewaleta pamoja wakuu wa nchi, Mawaziri na watoa maamuzi wa masuala ya nishati kutoka mashirika ya kimataifa, wadau wa kimataifa na wahusika binafsi lengo likiwa ni kutathmini maendeleo na kuainisha ajenda za utekelezaji ili kuharakisha mchakato wa dunia kuhamia katika matumizi ya nishati jadiifu.

UN /Kim Haughton

Tusijisahau, wakazi wa dunia wana matarajio makubwa na UN-Balozi Bande

Hatimaye kikao cha kwanza cha mkutano wa 74 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kimeanza leo kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani chini ya uongozi wa Rais wake Balozi Tijjani Muhammad-Bande kutoka Nigeria.

Kikao kilianza kwa Balozi Bande kugonga nyundo hiyo ya kuitisha wajumbe ili waketi tayari kwa shughuli za siku hiyo.

Kisha akatangazia wajumbe wasimame kwa dakika moja, ikiwa ni tamaduni ya kuanza kwa kikao kwa maombi na tafakuri.

Sauti
3'20"