Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

PETER CSOKA

Picha: FAO

Kuhifadhi na kupanua wigo wa misitu ni mtihani tunaotakiwa kushinda: FAO

Idadi ya watu ikiendelea kuongezeka duniani na kutarajiwa kufikia bilioni 9 mwaka 2050, kuhifadhi na kupanua wigo wa mistu kwa ajili ya kuwezesha kuwalisha watu hawa imekuwa mtihani ambao dunia inapaswa kuushinda kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa . 

Hayo yamesemwa leo na shirika la chakula na kilimo FAO kwenye mkutano wa kimataifa wa siku tatu unaofanyika Roma Italia kwa lengo la kuchukua hatua za pamoja miongoni mwa sekta ili kukomesha ukataji miti na kupanua wigo wa misitu. Suala ambalo linahitaji utashi wa kisiasa na hatua madhubuti .

Sauti
1'58"