Mlipuko wa volcano ya Tonga: Takribani watu watatu wamefariki dunia, wengine hawajulikani waliko
Takriban watu watatu wamefariki dunia nchini Tonga kufuatia mlipuko mkubwa wa volkano na wimbi la Tsunami lililotokea mwishoni mwa wiki. Nyumba na majengo mengine kote kwenye visiwa yamepata uharibifu mkubwa.