Skip to main content

Chuja:

Pakistani

09 JANUARI 2023

Ni Jumatatu ya tarehe 09 ya mwezi Januari mwaka 2023 na katika jarida la habari za umoja wa mataifa tunaangazia changamoto la mafuriko nchini Pakistan na kazi za walinda amani nchini DR Congo.  Makala tutakupeleka nchini Burundi na mashinani nchini Brazil.

Sauti
10'27"
Watu milioni 33 nchini Pakistani waliathiriwa na mafuriko makubwa yaliyokumba taifa hilo mwezi Septemba mwaka 2022
© WFP

Takribani watoto milioni 4 nchini Pakistani bado wanaishi kwenye maji machafu yaliyotwama- UNICEF

Nchini Pakistani, janga la uhai wa mtoto bado ni changamoto kubwa kwenye maeneo yaliyokumbwa na mafuriko zaidi ya miezi minne iliyopita huku idadi ya maambukizi  ya magonjwa ya hewa na utapiamlo uliokithiri au unyafuzi ikiendelea kuongezeka, limesema shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto,  UNICEF wakati huu ambapo jumuiya ya kimataifa inajiandaa kwa ajili ya mkutano wa kuchangia taifa hilo la Asia ili lijenge mnepo dhidi ya majanga.

Sauti
2'29"
Maeneo ya makazi yaliyofurika kwenye kijiji kimoja jimboni Sindh nchini Pakistan.
© UNICEF/Asad Zaidi

Ombi la kusaidia Pakistani laongezwa hadi dola milioni 816 kuepusha wimbi la pili la uharibifu

Wakati Pakistani ikihaha na kile kinachoitwa wimbi la pili la vifo na uharibifu kutokana na mafuriko makubwa yaliyokumba nchi hiyo mwezi Juni na kusababisha theluthi moja ya ardhi  ya taifa hilo kutwama, Umoja wa Mataifa umeongeza kiwango cha ombi la usaidizi wa kibinadamu kwa Pakistani kutoka dola milioni 160 hadi dola milioni 816.

Katibu Mkuu António Guterres (kushoto) alishuhudia athari za mafuriko katika majimbo ya Sindh na Balochistan. Akiwa huko, alikutana na watu walioathiriwa na mafuriko, pamoja na mashirika ya kiraia na watu waliofika mwanzo kusaidia.
UN Photo/Eskinder Debebe

Katibu Mkuu wa UN ashuhudia kiasi cha juu cha uvumilivu na ushujaa Pakistani 

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres, alipokuwa akihitimisha zaiara yake ya siku mbili nchini Pakistani Jumamosi ya Septemba 10, amesisitiza kwamba mahitaji katika Pakistan iliyokumbwa na mafuriko ni makubwa na akatoa wito wa msaada mkubwa na wa haraka wa kifedha, alipokuwa akihitimisha safari ya siku mbili yenye lengo la kuongeza ufahamu wa maafa yanayotokana na taianchi, anaripoti Shirin Yaseen wa UN News ambaye ni miongoni mwa waliosafiri na Katibu Mkuu. 

UN News/May Yaacoub

Katibu Mkuu wa UN ashiriki utoaji chanjo dhidi ya Polio Pakistani

Hii leo akiendelea na ziara yake nchini Pakistani, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ameshiriki katika kampeni  ya utoaji chanjo dhidi ya ugonjwa wa polio kwenye mji wa Lahore. Taarifa kamili na Brenda Mbaitsa

Kampeni hiyo ya kwanza ya kitaifa ya mwaka inayofanyika mwezi huu wa Februari inalenga kufikia zaidi ya watoto milioni 39 nchini humo katika taifa hilo ambamo mwaka jana pekee kulikuwepo na ongezeko kubwa la visa vya polio na polio pori mwaka jana na mwaka huu pekee tayari kuna wagonjwa 17.

Sauti
1'29"