UN yaonya dharura ya kibinadamu kuelekea msimu wa baridi Afghanistan baada ya tetemeko la ardhi
Kutokana na maafa yaliyosababishwa na tetemeko kubwa la ardhi katika majimbo ya Mashariki mwa Afghanistan, mashirika mawili ya Umoja wa Mataifa yametoa ombi la msaada la karibu dola milioni 40 kusaidia mamia ya maelfu ya watu walioathirika kwa ajili ya wakati msimu wa baridi unaokaribia.