Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya kuratibu misaada ya kibinadamu, OCHA leo imezungumzia hofu yake jinsi majanga na mizozo inavyoendelea kuwa kikwazo katika kukabiliana na mlipuko wa ugonjwa wa virusi vya Corona, COVID-19 huko Syria, Libya na Afghanistan huku ikipongeza hatua zilizochukuliwa na Sudan katika kukabiliana na kuenea kwa ugonjwa huo.