Wakimbizi wa Burundi wapewa vyeti vya kuzaliwa Tanzania
Asante Tanzania mwanangu sasa atajulikana alipozaliwa :Mkimbizi Evangeline
Familia za wakimbizi wa Burundi wanaoishi kwenye kambi ya Nyarugusu mkoani Kigoma nchini Tanzania wameishuru serikali ya taifa hilo la Afrika Mashariki kwa kuwapatia nyaraka muhimu za watoto wao, vyeti vya kuzaliwa wakati wa ziara ya Kamisha Mkuu wa wakimbizi Filippo Grandi iliyokamilika mwishoni mwa wiki. Happiness PPalangyo na taarifa zaidi