MONUSCO yaendelea na doria wakati mapigano yakianza tena kati ya M23 na FARDC, Kivu Kaskazini
Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC mapigano kati ya jeshi la serikali FARDC na waasi wa kundi la M23 yalianza tena jana Jumapili kwenye eneo la Kibumba jimboni Kivu Kaskazini mashariki mwa taifa hilo.