Tuzo ya UNCTAD imenipa motisha zaidi kusaidia jamii – Dkt Julian Omalla
Mshindi wa tuzo ya wanawake wajasiriamali iliyotolewa na Kamati ya Umoja wa Mataifa ya biashara na maendeleo, UNCTAD na pia akapigwa jeki ya mkopo nafuu wa dola milioni 10 kutoka kwa serikali ya Uganda ameeleza alivyopokea tuzo hiyo na mipango ya baadaye. Akizungumza na mwandishi wetu wa Uganda John Kibego, Dkt Julian Omalla ambaye amejipatia umaarufu kutokana na shughuli za kujikwamua pamoja na maelfu ya wanawake na vijana, amesema amepata maono makubwa zaidi baada ya kutunikiwa tuzo.