UN yataka kila nchi itie saini kutofanya majaribio ya silaha za nyuklia
Ikiwa leo ni siku ya kimataifa ya kupinga majaribio ya silaha za nyuklia Rais wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa Csaba Kőrösi amesema kitendo cha matumizi ya kijeshi duniani kufikia dola trilioni 2.2 mwaka 2022 si ishara nzuri kwa usalama wa dunia na kutoa wito wa utashi wa kisiasa kwa nchi zote katika kuhakikisha dunia haina matumizi ya silaha za nyuklia.