Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

NPT

Watu wakiandamana kupinga silaha za nyuklia katika  mkutano wa mabadiliko ya tabianchi huko Geneva. (maktaba)
ICAN/Lucero Oyarzun

UN yataka kila nchi itie saini kutofanya majaribio ya silaha za nyuklia

Ikiwa leo ni siku ya kimataifa ya kupinga majaribio ya silaha za nyuklia Rais wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa Csaba Kőrösi amesema kitendo cha matumizi ya kijeshi duniani kufikia dola trilioni 2.2 mwaka 2022 si ishara nzuri kwa usalama wa dunia na kutoa wito wa utashi wa kisiasa kwa nchi zote katika kuhakikisha dunia haina matumizi ya silaha za nyuklia. 

Majeruhi baada ya kukimbia moto uliotokana na bomu la atomiki lililoangushwa saa 2.15 asubuhi, walikusanyika kwenye kingo ya barabara magharibi mwa Miyuki-bashi mjini Hiroshima saa tano asubuhi ya tarehe hiyo hiyo ya shambulio 6 Agosti 1945.
UN /Yoshito Matsushige

“Hibakusha” ni ishara ya kile UN inasimamia kutokomeza nyuklia- Guterres

Miaka 76 imetimu hii leo tangu Marekani iangushe bomu la nyuklia katika mji wa Hiroshima nchini Japan na kuua makumi ya maelfu ya watu papo hapo, bado hatua za kutokomeza silaha za nyuklia zinasuasua, hivyo serikali chukueni hatua kufanikisha lengo hilo. Takwimu zinaonesha kuwa watu wengine makumi ya maelfu walifariki dunia baadaye na wengine wengi miaka iliyofuatia.
 

UN Photo/Eskinder Debebe)

Hatua ya DPRK ni ya kuungwa mkono

Vitisho vya matumizi ya nyuklia kwa makusudi au vinginevyo vinaongezeka hivi sasa na kuleta changamoto kama ilivyokuwa miaka 50 iliyopita wakati mkataba wa kudhibiti kuenea kwa silaha duniani, NPT ulipopitishwa.

Mwakilishi wa ngazi ya juu wa Umoja wa Mataifa kuhusu kudhibiti matumizi ya silaha, Izumi Nakamitsu amesema hayo leo mjini Geneva, Uswisi mwanzoni mwa kikao cha mapitio ya awali ya mkataba huo.

Amesema vitisho hivyo vitaendelea kuwepo iwapo mataifa yataendelea kuhifadhi silaha hizo akitolea mfano maeneo ya rasi ya Korea.

Sauti
1'22"