Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Njombe

Mkoani Njombe kusini mwa Tanzania, mapishi mbalimbali kutokana na matumizi ya mikunde. Hii inafuatia mafunzo yaliyowezeshwa na FAO na AgriConnect.
FAO Tanzania

Nyama ikiingia mezani, mikunde hunyanyapaliwa- FAO

Jamii ya mikunde! Wengi wanaitambua zaidi kama ni kunde zenyewe, na maharagwe lakini ni zaidi ya hiyo. Kuna choroko, mbaazi, dengu, njegere na kadha wa kadha ambapo kutokana na umuhimu wake sio tu kiuchumi bali pia katika lishe ya binadamu, kurutubisha udongo na pia kuhimili mabadiliko ya tabianchi, ndio maana Umoja wa Mataifa unapigia chepuo.

Sauti
4'55"
UN News

Kulima tunalima lakini lishe bado ni changamoto tuchukue hatua- Mkulima Sarah

Jamii ya mikunde! Wengi wanaitambua zaidi kama ni kunde zenyewe, na maharagwe lakini ni zaidi ya hiyo. Kuna choroko, mbaazi, dengu, njegere na kadha wa kadha ambapo kutokana na umuhimu wake katika lishe ya binadamu, kurutubisha udongo na pia kuhimili mabadiliko ya tabianchi, ndio maana Umoja wa Mataifa unapigia chepuo.

Mathalani nchini Tanzania, shirika la Umoja wa Mataifa la chakula na kilimo, FAO linafadhili mradi wa AgriConnect ambao pamoja na mambo mengine  unapatia wananchi, wake kwa waume stadi za mapishi sahihi ya jamii ya mikunde.

Sauti
4'55"

22 FEBRUARI 2023

Hii leo jaridani tunakuletea habari kuhusu mwelekeo wa matumizi ya maji barani Afrika, na elimu kwa watoto waliotumikishwa jeshini nchini DR Congo.  Makala tutakupeleka nchini Tanzania na mashinani tunarudi tena nchini DR Congo.

Sauti
11'41"
Photo FAO/Marco Salustro

Matunda ni lishe muhimu katika mlo wa kila siku

Emmanuel Mwanjisi ni Afisa lishe kutoka hospitali ya Consolatha, Ikonda, katika wilaya ya Makete, nyada za juu kusini mwa Tanzania, akieleza faida za ulaji wa mbogamboga na matunda katika mwili wa binadamu ameeleza kuwa wataalamu wa lishe wanapohamasisha ulaji wa matunda hawamaanishi kuwa ni lazima mlaji ale kiasi kikubwa cha matunda hayo bali kiasi chochote hata kipande kidogo lakini mara kwa mara, kinasaidia kuleta faida mwilini. 

Sauti
3'50"
© FAO/Miguel Schincariol

Ulaji wa mbogamboga na matunda siyo suala la kipato, ni uelewa. 

Mkoa wa Njombe, ni miongoni mwa mikoa iliyoko nyanda za juu kusini mwa Tanzania. Eneo hili linatajwa kuwa lenye rutuba ambalo lina mazingira mazuri ya kuweza kustawisha mbogamboga na matunda ya aina mbalimbali kama vile matufaa, parachichi na mengine mengi. Laicha ya hali hiyo, mkoa huu ni miongoni mwa maeneo yenye watu wenye utapiamlo, ukitajwa kuwa na asilimia 53.6 ya watu wake wenye utapiamlo.  

Sauti
4'2"
UN News

Haki za watoto ni haki za binadamu lazima ziheshimiwe:UNICEF

Haki za watoto ni haki za binadamu na zinapaswa kuheshimiwa na kutekelezwa katika kila ngazi kuanzia kwenye familia, jamii na hata serikali kwa mujibu wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF. Hata hivyo shirika hilo linasema mara nyingi hazitekelezwi hususan suala la ukatili, kuwatelekeza, mimba za utotoni  na hata kutowapa elimu. Nchini Tanzania serikali imelivalia njuga suala hilo likitaka kila kijiji, wilaya na mkoa kuchukua hatua kuhakikisha haki hizo zinatambuliwa na kuzingatiwa kwa kushirikisha wadau wote katika jamii wakiwemo mashirika yasiyo ya kiserikali.

Sauti
4'47"