Ujio wa ‘Jopo la kuhama kutoka mafuta ya kisukuku’ watangazwa kwenye COP28
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres leo Jumamosi ametangaza mpango wake wa kuunda jopo linalolenga kuhakikisha hatua za kuondoka katika matumizi ya nishati ya mafuta ya kisukuku kuelekea nishati mbadala zinakuwa za haki, endelevu na kunufaisha nchi zote.