Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Nishati mbadala

UNCDF

Ushirikiano wa UNCDF na wananchi wa Ikungi Tanzania waleta mabadiliko chanya

Kuanzia wiki hii viongozi wa ulimwengu wanamiminika jijini New York Marekani kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa kushiriki Mkutano wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa. Mambo kadhaa yatajadiliwa ikiwemo amani, haki za binadamu, uchumi na kuilinda sayari dunia dhidi ya uharibifu unaochochea majanga. Ulimwengu tayari umebaini kuwa changamoto zimefungana na hivyo majawabu yanapaswa kutafutwa kwa kushirikiana. Katika maeneo ambayo ushirikiano umefanyika ili kutafuta ufumbuzi wa jambo, matunda yameonekana.

Sauti
4'3"
Paneli za nishati ya jua zikitumika nchini Cambodia ili kufikia hitaji la nishati la nchi hiyo.
UNDP/Manuth Buth

Mjadala wa aina yake wa ngazi ya juu kuhusu nishati unaofanyika Ijumaa hii, haujapata kutokea kwa takribani miaka 40  

Sambamba na azimio la Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa namba 74/225, Katibu Mkuu Ijumaa hii ya tarehe 24 Septemba ameandaa mjadala wa ngazi ya juu wa Nishati wakati huu wa Mjadala Mkuu wa ngazi ya juu wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa UNGA76 ili kuharakisha utekelezaji wa lengo namba 7 la maendeleo endelevu linalohusiana na nishati endelevu.  

UNICEF/Tanya Bindra

Mwanamke ajikwamua kwa juhudi zinazojali mazingira, Uganda

Wakati ulimwenguni kukishuhudiwa mabadiliko ya tabianchi na athari zake Umoja wa Mataifa unahimiza nchi na watu binafsi kushiriki katika kuyalinda mazingira kwa njia mbali mbali ikiwemo kugeuza athari kuwa faida. Uchafuzi wa hewa na ukataji miti ni miongoni mwa changamoto ambazo zinajitokeza katika utunzaji wa mazingira. Lakini nchini Uganda baadhi ya watu wameanza kupata mwamko na kutambua kuwa wasipohifadhi mazingira leo basi vizazi vya kesho viko mashakani. Miongoni mwao ni mwanamke mmoja aliyeamua kutumia nishati mbadal ambayo inajali mazingira, kulikoni?

Sauti
3'48"

Kutoka kuwa wakili mahakamani hadi kuuza mkaa

Vijana! Vijana! Vijana! Umoja wa Mataifa unasema ndio mkombozi wa kizazi cha sasa na kijacho hasa katika kuepusha dunia hii na madhara ya mabadiliko ya tabianchi yanayochochewa na mambo kadhaa ikiwemo ukataji miti kwa ajili ya mkaa. Ni kwa kutambua hilo, kijana mmoja nchini Tanzania wakati akisoma shahada yake ya kwanza ya sheria kwenye Chuo Kikuu, alibonga bongo ya jinsi ya kuondokana na mkaa unaoharibu mazingira. Alikuja na wazo lake ambalo katika sehemu hii ya kwanza ya mahojiano na Assumpta Massoi anaelezea safari yake na anaanza kwa kujitambulisha.

Sauti
4'15"

Nishati ya kupikia bado ni mtihani mkubwa kwa wanawake Ziwa Albert

Upatikanaji wa nishati ya kupikia ambayo ni moja ya mahitaji ya msingi bado unakabiliwa na changamoto wakati huu ambapo kuna mwamko kuhusu umuhimu wa kulinda mazingira na kutumia nishati mbadala.  

Mila na desturi katika jamii pia zinaonekana kuchangia katika kuongeza shinikizo zinazokabili wanawake katika kusaka kuni hususan maeneo ya vijijini ambako upatikanaji wa nishati mbadala ni ngumu.

Sauti
3'50"