Skip to main content

Chuja:

nishati endelevu

06 JUNI 2023

Jaridani hii leo tunaangazia ni mada kwa kina na nakupeleka mwambao wa Ziwa Tanganyika nchini Tanzania, hususan mkoani Rukwa ambako huko utasikia harakati za Umoja wa Mataifa za kujumuisha wanawake kwenye uvuvi. Pia tunakuletea habari kwa ufupi zikiwemo za Nishati jadidifu, mabadiliko ya tabianchi na afya. Katika mashinani tunakupeleka nchini Sudan Kusini kusikia ni kwa jinsi gani vijana wanachangia katika mchakato wa utengenezaji wa katiba ukielekea uchaguzi mkuu nchini humo.

Sauti
13'27"
Paneli za nishati ya jua zikitumika nchini Cambodia ili kufikia hitaji la nishati la nchi hiyo.
UNDP/Manuth Buth

Mjadala wa aina yake wa ngazi ya juu kuhusu nishati unaofanyika Ijumaa hii, haujapata kutokea kwa takribani miaka 40  

Sambamba na azimio la Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa namba 74/225, Katibu Mkuu Ijumaa hii ya tarehe 24 Septemba ameandaa mjadala wa ngazi ya juu wa Nishati wakati huu wa Mjadala Mkuu wa ngazi ya juu wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa UNGA76 ili kuharakisha utekelezaji wa lengo namba 7 la maendeleo endelevu linalohusiana na nishati endelevu.  

UN Photo/Isaac Billy

Nishati ya Ethanol itakuwa mbadala wa mkaa-UNIDO Tanzania

Nishati ya ‘Ethanol’ inayotokana na masalia ya vitu mbalimbali kwa mfano mazao kama miwa, mahindi, viazi na hata ngano ni moja ya suluhisho linaloonekana kuwa mjarabu kwa uharibifu wa mazingira unaosababishwa na matumizi ya nishati kama mkaa. Malengo mbalimbali ya maendeleo endelevu SDGs likiwemo lile la 7 linalohamasisha nishati, yanasisitiza uwekezaji katika mbinu mbadala kama hizo za ethanol ili kuifanya dunia kuwa mahali pazuri pa kuishi na hivyo kufanikisha  utimizaji wa SDGs ifikapo mwaka 2030.

Sauti
3'43"