Mabadiliko ya tabianchi yanazidi kuongeza idadi ya wakimbizi wa ndani:UNHCR
Shirika la Umoja wa Mataifa linalohudumia Wakimbizi UNHCR, limetahadharisha ongezeko la wakinbizi huko Sahel na kutoa ombi la msaada wa haraka wa mahitaji ya kibinadamu kwa zaidi ya watu milioni 3.4 waliokimbia makazi yao na wenyeji wao kutokana na mafuriko makubwa yaliyozikumba nchi za Nigeria, Chad, Niger, Burkina Faso, Mali na Cameroon hivi karibuni.