Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

niger

Wanawake na watoto wakisubiri mgao wa chakula kutoka WFP nchini Niger
© WFP/Mariama Ali Souley

Miradi ya kujenga mnepo ni muhimu iendelee Niger hata katikati ya janga la kisiasa- WFP

Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Maendeleo ya Chakula duniani, WFP linasema kadri vurugu za kisiasa zikizidi kutikisa Niger, harakati za kuendeleza hatua za muda mfupi na muda mrefu za kukabili njaa inayoshamiri kila uchao nchini humo ni muhimu zaidi. Msaada wa dharura kutoka WFP unahitajika kufikia watu pindi wanapohitaji msaada huo na kwa kiwango kinachotakiwa. Ni kwa mantiki hiyo WFP inataka watumishi wa usaidizi wa kiutu pamoja na vifaa wanavyosafirisha vipate ruhusa ya kupita bila vikwazo vyovyote, upatikanaji wa fedha uwe wa uhakika, halikadhalika kuendelea kwa migao ya vyakula na miradi ya maendeleo.

 

 

UN News/ Hisae Kawamori

Manusurua kutoka Gambia: Sitamani tena kuzamia kwenda ulaya

Kila mwaka maelfu ya wahamiaji kutoka maeneo mbalimbali ikiwemo Afrika hujaribu kufika Ulaya wakivuka Bahari ya Mediterania wakieleza kwenda kusaka maisha bora lakini safari hiyo inaelezwa kuwa ni hatari sana kwani maelfu ya watu hufa maji au kutoweka. 

Ni Amadou Jobe kijana ambaye akiwa na umri wa miaka 25 alianza safari ya hatari kutoka nchini Kwake Gambia kupitia kaskazini mwa Afrika lengo likiwa Kwenda nchini Italia kusaka maisha bora kwani alikuwa akiishi katika hali ya umasikini na alitamani kuja kuisaidia familia yake iwapo angefanikiwa kufika Ulaya. 

Sauti
3'19"

27 JULAI 2023

Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina ambapo Jacqueline Woiso, Mkurugenzi Mwendeshaji wa Multichoice Tanzania anafafanua ni malengo yapi ya Maendeleo Endelevu yaliyoipa Multichoice Tanzania Ushindi wa Tuzo ya UN Global Compact. Pia tunakuletea habari kwa ufupi zikiwemo ripoti ya hali ya hewa, jaribio la kutaka kutwaa madaraka kijeshi nchini Niger na uhifadhi wa bioanuwai barani Afrika. Katika kujifunza lugha ya Kiswahili tunakuletea maana ya neno “NDOFYA". 

Sauti
10'