Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Nicaragua

30 DESEMBA 2020

Katika Jarida la Umoja wa Mataifa hii leo Flora Nducha anakuletea matukio ya mwaka 2020

-Mwaka 2020 ulitangazwa kuwa mwaka wa wauguzi na wakunga na shirika la afya duniani WHO

-Janga la corona au COVID-19  Machi mwaka huu lilitangazwa kuwa janga la kimataifa. Na kwa mujibu wa WHO nchi 222 duniani zimeathirika huku watu zaidi ya milioni 1 na laki 7 wakipoteza maisha na wengine zaidi ya milioni 79 wameambukizwa ugonjwa huo

Sauti
11'45"
OHCHR Regional Office for Centra

Catalina:Tunataka watambue kuwa kuna binadamu wanaojali binadamu wenzao

Catalina, si jina lake halisi, ni mwanasheria kutoka Nicaragua mwenye umri wa miaka 44 na ambaye alikimbilia nchi jirani ya Costa Rica ili kunusuru maisha yake na ya watoto wake wawili. Flora Nducha na maelezo zaidi.

Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR linasema kuwa Catalina hivi sasa ni mkimbizi Costa Rica. 

Mwaka 2018 wakati wa maandamano dhidi ya serikali nchini Nicaragua, Catalina alifungua milango ya nyumba yake ili kusaidia waandamanaji ambapo aliwapatia chakula pamoja na huduma ya kwanza pindi walipopata majeruhi. 

Sauti
2'21"
Wanicaragua wakiwa wanasubiri kufanya maombi ya hifadhi katika ofisi ya uhamiaji katika mji mkuu wa Costa Rica, San Jose (Agosti 2018)
UNHCR/Roberto Carlos Sanchez

Mwaka mmoja wa mgogoro wa Nicaragua, zaidi ya watu 60,000 wameikimbia nchi.

Msemaji wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuwahudumia wakimbiazi UNHCR Liz Throssell amewaambia wana habari hii lemjini Geneva Uswisi kuwa inakadiriwa kuwa watu wapatao 62,000 wameikimbia Nicaragua na kusaka hifadhi katika nchi za jirani wengi wao kufikia 55,500 wakiingia Costa Rica kutokana na mazingira magumu nchini mwao tangu mwaka jana.