Ushiriki wa wanawake katika utoaji na ufikishaji wa misaada Afghanistan lazima uendelee: UN na wadau
Uamuzi wa mamlaka ya Afghanistan wa kuwapiga marufuku wanawake kufanya kazi katika mashirika ya kibinadamu yasiyo ya kiserikali NGO’s umeendelea kulaaniwa na wadau mbalimbali kutoka jumuiya ya kimataifa yakiwemo mashirika ya Umoja wa Mataifa wakisema ni pigo kubwa kwa jamii zilizo hatarini, kwa wanawake, kwa watoto, na kwa nchi nzima kulingana.