Nepal yateua Waziri Mkuu wa kwanza mwanamke, huku UN ikionesha mshikamano
Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini Nepal yamekaribisha uteuzi wa Sushila Karki kuwa Waziri Mkuu wa mpito, wakati nchi hiyo ikikumbwa na mshtuko kufuatia ukandamizaji wenye umwagaji damu dhidi ya maandamano yaliyoongozwa na vijana, ambayo yalisababisha vifo vya zaidi ya watu 50, uharibifu mkubwa wa mali na kujiuzulu kwa mtangulizi wake.