Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Nepal

Navesh Chitrakar

Türk ataka uwajibikaji wa vikosi vya usalama Nepal na waandamanaji wazingatie kanuni

Kamishna Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusu Haki za Binadamu ameonesha wasiwasi mkubwa kufuatia ghasia zinazoendelea na kushika kasi nchini Nepal, huko barani Asia, ambako maandamano dhidi ya ufisadi na marufuku ya mitandao ya kijamii yamesababisha vifo vya watu wengi pamoja na majeruhi. Flora Nducha amefuatilia taarifa hiyo na anatupasha zaidi.

Kamishna wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa, Volker Türk, akizungumza mjini Geneva amesema

Sauti
2'49"

10 SEPTEMBA 2025

Leo jaridani Assumpta Massoi anamulika kauli ya OHCHR kufuatia maandamano yanayoendelea Nepal; Utipwatipwa 'wapiku' utapiamlo na harakati za kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi huko Karamoja nchini Uganda,

Sauti
10'18"

29 AGOSTI 2025

Jaridani leo tunaangazia Majaribio ya Nyuklia, na machafuko nchini Sudan Kusini. Makala tunakwenda nchini Nepal na mashinani tunasalia huko huko Sudana Kusini, kulikoni?

Sauti
9'50"

22 APRILI 2025

Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina ambayo inatupeleka Msasani nchini Tanzania kusikia namna vijana na serikali wanavyolinda Mama Dunia. Pia tunakuletea muhtasari wa habari ujumbe wa Katibu Mkuu, watoto kulinda mazingira DRC, na kifo cha Papa Francis.

Sauti
9'56"
Fermín alikuwa mtu wa kwanza katika jumuiya yake kutengeneza choo, kutokana na kampeni ya UNICEF Colombia na Wakfu wa Kimataifa wa Baxter.
© UNICEF/Colombia

Siku ya Choo Duniani: Tumia ubunifu kwa usafi na mazingira salama

Ubunifu umeenea katika mbio za kupanua upatikanaji wa maji safi na usafi wa mazingira duniani kote wakati dunia ikiadhimisha Siku ya Choo Duniani, hii leo tarehe 19 Novemba.

Sambamba na kaulimbiu ya mwaka huu ya kuongeza kasi ya mabadiliko, wavumbuzi wamekuwa sehemu ya juhudi zinazoendelea kushughulikia mahitaji ya takriban watu bilioni 3.5 duniani wanaoishi bila vyoo salama.