Skip to main content

Chuja:

nairobi

01 SEPTEMBA 2023

Hii leo jaridani tunaangazia mabadiliko ya tabianchi na malelengo ya maendeleo endelevu kupitia mchezo wa mpira wa miguu. Makala tutaelekea nchini DRC kusikia simulizi ya wakimbizi na mashinani tunakupeleka nchini Tanzania kusikia ni kwa vipi wanawake wameweza kufanya kazi zao na kunyonyesha watoto wao ipasavyo.

Sauti
12'14"
UN SDGs

Vijana wanaweza kuchagiza SDGs ikiwa watapewa miongozo sahihi - Austine Oduor

Vijana wanaaminika kuwa kundi muhimu katika kufanikisha malengo ya maendeleo endelevu, SDGs kwani nguvu yao ikikutana na ubunifu, inaweza kufanikisha mambo mengi chanya kwa ulimwengu. Hata hivyo kundi hili likikosa miongozo na taarifa sahihi linaweza kuwa kikwazo cha maendeleo yanayotarajiwa. Ndio maana Austine Oduor wa nchini Kenya, aliamua kuanzisha miradi inayowasaidia vijana wa mtaa wa mabanda wa Mukuru kwa Njenga jijini Nairobi, Kenya ili waweze kuanzisha biashara zao na pia kuwapa ushauri kuhusu maisha bora kuwaepusha na uhalifu.

Sauti
3'17"
UN/ Jason Nyakundi

Kilio cha sodo au taulo za kike kwa wasichana Nairobi, Kenya chapatiwa jibu

Shirika la Umoja wa Mataifa la idadi ya watu duniani, UNFPA linapatia msisitizo suala la wanawake na wasichana kupata taulo za kike au sodo, kwa kuzingatia kuwa ni suala la haki za binadamu. Ukosefu wa vifaa hivyo siyo tu vinashusha utu na hadhi ya mtu pale anapojikuta amechafua nguo zake mbele za hadhira, bali pia humkosesha haki ya kuwa huru kwenda kazini, shuleni. Katika maeneo ya mitaa ya mabanda jijini Nairobi nchini Kenya, wanawake na wasichana wanaoshi katika lindi la umaskini, sodo au taulo za kike ni changamoto kubwa.

Sauti
3'45"
World Bank/Sambrian Mbaabu

Niliyaishi maisha ya kurandaranda mitaani, ninafahamu wanachokipitia. 

Tangu umri wa takriban miaka 6 Joseph Njoroge Wanyoike aliishia kuwa mtoto wa kurandaranda mitaani mjini Nairobi. Kutokana na mkono wa msamaria mwema, Joseph amefanikiwa katika maisha na sasa ameamua naye kurejesha kwa jamii. Kwa sasa Joseph Njoroge anamiliki kituo cha kuwatunza na kukuza vipaji  vya vijana wa kurandaranda mitaani vikiwemo vya kucheza soka katika mji mdogo wa Ngong’ nje ya mji wa Nairobi.  Mwandishi wa Kenya Jason Nyakundi amezungumza naye kutaka kufahamu safari yake

Sauti
3'37"
© UN-Habitat /Julius Mwelu

Wakazi wa Mathare nchini Kenya washukuru UNICEF kwa kuwawekea tenki za maji

Maambukizi mapya ya ugonjwa wa virusi vya Corona au COVID-19, yakiendelea kuripotiwa nchini Kenya, shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF nchini humo limeanzisha zaidi ya vituo 1000 vya kunawa mikono katika eneo la makazi duni la Mathare kwenye mji mkuu Nairobi, kama njia mojawapo ya kukabiliana na maambukizi mapya. Loise Wairimu na ripoti kamili.

Eneo hili la Mathare, jijini Nairobi nchini Kenya, lenye zaidi ya wakazi 200,000 [Laki Mbili] ambao uhaba wa maji safi na salama kwenye eneo hilo ni mwiba katika kutokomeza COVID-19.

Sauti
2'15"

10 JUNE 2020

Jaridani la Umoja wa Mataifa hii leo:
-  Nchini Kenya Wagonjwa wasio na dalili kali za COVID-19 kutibiwa nyumbani
- Wakazi wa Mathare nchini Kenya washukuru UNICEF kwa kuwawekea tenki za maji
- UNICEF yachukua hatua kukabiliana na ukatili wa kingono Sierra Leone
-Na kwenya mashinani tunabisha hodi Nigeria kwa mwanariwanya mashuhuri Chimamanda Adichie Ngozi  nazungumzia jinsi ya kuondoa fikra potofu za wanaume juu a umiliki wa miili ya wanawake
-Na kwenye makala hii leo tuko katika Shule Kuu ya Uandishi wa Habari na Mawasiliano kw
Sauti
13'42"
UN-Habitat/Julius Mwelu

Kijana kutoka Nairobi Kenya aupa kisogo uhalifu na sasa anajihusisha na utunzaji wa mazingira

Kutana na Fredrick Okinda ni mmoja wa vijana waliokuwa wahalifu sugu katika mtaa wa mabanda wa Korogocho ulio mjini Nairobi, Kenya. Kama wahenga walivyonena kufanya kosa si kosa kosa kubwa ni kurudia kosa. Amejifunza kutokana na makossa na kuamua kubadili Maisha yake na ya vijana wenzie waliopitia njia kama yake. Kwa sasa Fredrick ni kiongozi wa kikundi kwa jina Kombgreen Solutions kinachowaleta pamoja vijana walio katika uhalifu, kuwasaidia kubadili tabia na kushiriki katika huduma za jamii hasa utunzi wa mazingira.

Sauti
3'43"
Picha: Kwa hisani ya James Waikibia

Maji safi na maji taka vyote ni changamoto Nairobi Kenya

Uondoaji  wa maji taka na upatikanaji wa maji safi ya kunywa vyote ni changamoto kubwa ambayo inakumba sehemu  nyinyi na hasa miji ya nchi za Afrika. Kila mara mabomba ya maji taka hupasuka na kuvuja ambapo na ukarabati wa miundo mbinu muhimu kama hiyo  huchukua muda mrefu na wakati mwingine kutelekezwa kabisa.

Sauti
4'32"