Kampeni dhidi ya kipindupindu yaimarishwa huko Khartoum nchini Sudan
Shirika la afya ulimwenguni, WHO, linashirikiana na wadau wake kusaidia kuepusha kuenea zaidi kwa mlipuko wa ugonjwa wa Kipindupindu kwenye jimbo la Khartoum nchini Sudan ikiwemo mji mkuu Khartoum. Brenda Mbaitsa na ripoti kamili.
Mwakilishi wa WHO nchini Sudan Dkt. Naeema Al Gasseer amenukuliwa katika taarifa iliyotolewa leo mjini Khartoum akisema kuwa hatua ya shirika hilo inafuatia ombi la Waziri wa Afya wa Sudan Dkt. Akram Eltoum.