Mamia ya wanafunzi katika mji wa pili kwa ukubwa nchini Msumbuji wa Beira wanaendelea kusoma katika madarasa yasiyo na paa hali aliyoishuhudia Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres anayeendelea na ziara nchini humo akizungumza na makundi mbalimbali ya waathirika wakiwemo watu wenye ulemavu.