Wakati hofu ikiendelea kutanda kuhusu idadi ya visa vilivyoripotiwa kutokana na mlipuko wa virusi vipya vya Corona na pia kusambaa kwake katika nchi 18 hivi sasa, shirika la umoja wa Mataifa la uhamiaji IOM limesema liko tayari kutoa msaada wa kiufundi kwa serikali likishirikiana na shirika la afya ulimwenguni WHO ili kuwawezesha watu kusafiri katika njia salama kiafya na kusaidia utekelezaji wa hatua za afya za kijamii ili kuhakikisha athari ndogo katika jamii na uchumi.