Tatizo la wakimbizi ni jukumu la kila mtu sio wakimbizi au nchi zinazowahifadhi pekee, kwani nimejifunza ukarimu sio lazima uendane na utajiri. Hayo yamesemwa na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa hii leo katika kongamano la kimatifa kwa ajili ya wakimbizi linaloendelea mjini Geneva Uswis.
Mpango jumla wa hatua za kibinadamu nchini Syria unahitaji karibu dola bilioni 3.3 na kwa sasa umefadhiliwa kwa asilimia 52 kwa jumla, kwa mujibu wa msemaji wa OCHA Jens Laerke.
Mvua kubwa isiyo ya kawaida na mafuriko yamezidi kukumba Somalia, Sudan Kusini na Kenya mwaka huu. Watabiri wa hali ya hewa wanatarajia mvua hiyo kubwa kuendelea kunyesha hadi Desemba.
Shirika la Umoja wa Mataifa la uhamiaji IOM leo limelaani vikali mauaji ya wahudumu watatu wa misaada ya kibinadamu wa shirika hilo yaliyofanyika Jumapili kwenye jimbo la Equatoria ya Kati nchini Sudan kusini.
Timu ya wahudumu wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR iliyoko Kaskazini mwa Iraq imeripoti kwamba jana usiku wakimbizi zaidi ya 900 kutoka Syria wamewasili katika kambi ya Bardarash kwa kutumia mabasi 45 na kufanya idadi ya wakimbizi katika kambi hiyo kufikia 9,700.
Takwimu mpya kufuatia shughuli ya mgao wa chakula mwezi Agosti zinaonyesha kuwa shirika la mpango wa chakula duniani, WFP, lilifikia rekodi mpya kufikishia chakula watu milioni 12.4, wanaokumbwa na uhaba wa chakula mwezi Agosti.
Serikli ya Uchina leo imetia saini makubaliano ya kuchangia dola milioni moja kwa shirika la Umoja wa Mataifa la msaada wa wakimbizi wa Kipalestina UNRWA.
Jumla ya dola milioni 50 zinahitajika hraka ili shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula duniani WFP liweze kufanya maandalizi muhimu kwa ajili ya kukabiliana na mlipuko wa Ebola unaoendelea nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC na uwezekano wa mlipuko katika nchi jirani.
Jumla ya dola milioni 50 zinahitajika hraka ili shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula duniani WFP liweze kufanya maandalizi muhimu kwa ajili ya kukabiliana na mlipuko wa Ebola unaoendelea nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC na uwezekano wa mlipuko katika nchi jirani.