WHO yatoa msaada wa magari ya kubeba wagonjwa 20 kusaidia sekta ya afya Ukraine
Katika kusaidia huduma ya afya nchini Ukraine, shirika la Umoja wa Mataifa la afya ulimwenguni WHO limetoa msaada wa magari ya kubeba wagonjwa 20 ili kuiwezesha sekta ya afya kutoa huduma katika maeneo yaliyoathiriwa na ambayo hayafikiki kutokana na vita nchini humo.