UN yaingiwa hofu kufuatia Urusi kusitisha ushiriki wake kwenye makubaliano ya usafirishaji nafaka Bahari Nyeusi
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, António Guterres ameelezea wasiwasi wake mkubwa juu ya uamuzi wa Urusi kusitisha ushiriki wake kwenye makubaliano ya usafirishaji nafaka kupitia Bahari Nyeusi, au kwa kiingereza, Black Sea Grain Initiative, makubaliano ambayo yalianzishwa tarehe 22 mwezi Julai mwaka huu ili kuwezesha Ukraine kuanza kuuza tena nje ya nchi hiyo vyakula na mbolea.