Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Mpango wa Nafaka katika Bahari Nyeusi

Meli ya kwanza ya kibiashara ikiwa na nafaka kupitia mpango wa usafirishaji wa nafaka kupitia Bahari Nyeusi
© UNOCHA/Levent Kulu

UN yaingiwa hofu kufuatia Urusi kusitisha ushiriki wake kwenye makubaliano ya usafirishaji nafaka Bahari Nyeusi

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, António Guterres ameelezea wasiwasi wake mkubwa juu ya uamuzi wa Urusi kusitisha ushiriki wake kwenye makubaliano ya usafirishaji nafaka kupitia Bahari Nyeusi, au kwa kiingereza, Black Sea Grain Initiative, makubaliano ambayo yalianzishwa tarehe 22 mwezi Julai mwaka huu ili kuwezesha Ukraine kuanza kuuza tena nje ya nchi hiyo vyakula na mbolea.

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres akiwa katika meli ya majaribio kupitia bahari ya Marmara nchini Uturuki ili kumtazama Kamanda Jasiri.
UN Photo/Mark Garten

Kama ilivyo kwa Nafaka, Mbolea pia inahitajika katika soko la dunia: Guterres

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres hii leo nchini Uturuki ametembelea na kukagua shughuli zinazoendelea za ukaguzi wa meli kutoka Ukraine zenye shehena ya nafaka zinazoenda kuuzwa katika soko la kimataifa na kupongeza muungano wa wakaguzi hao kutoka Ukraine , Urusi, Uturuki na Umoja wa Mataifa kwa kazi nzuri wanayofanya ambayo itasaidia dunia kuondokana na upungufu wa chakula uliosababisha bei kupanda na kuathiri zaidi nchi zinazoendelea zenye rasilimali chache kuweza kukidhi mahitaji ya wananchi wake.