Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Moussa Faki Mahamat

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres (Kulia) na mwenyekiti wa tume ya Muungano wa Afrika Moussa Faki Mahamat wakihutubia waandishi wa habari.
Video Screen Shot

Kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi, usalama na amani ni muhimu katika kufikia maendeleo Afrika-AU, UN

Mabadiliko ya tabianchi ni moja ya masuala ambayo yataathiri ukuaji wa uchumi wa bara Afrika iwapo uchafuzi wa mazingira hautapunguzwa kwa asilimia 45 kufikia mwaka 2030 na kutokomezwa kabisa ifikapo mwaka 2050 amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres akihutubia waandishi wa habari Jumatatu alasiri jijini New York, Marekani.

MONUSCO Forces/FIB-TANZBATT

Walinda amani wa Afrika wanalinda dunia nzima- Guterres

Umoja wa Mataifa, UN na Muungano wa Afrika, AU wameelezea wasiwasi wao mkubwa juu ya sintofahamu inayoendelea kukumba mfumo wa dunia na kusababisha madhara kwenye amani na usalama duniani.

Katibu Mkuu wa UN Antonio Guterres na Mwenyekiti wa kamisheni ya AU Moussa Faki Mahamat wamesema hayo katika taarifa yao ya pamoja waliyoitoa mwishoni mwa mkutano wa pili wa kila mwaka wa vyombo hivyo viwili mjini Addis Ababa nchini Ethiopia hii leo.

Wamesema kila nchi inapaswa kuzingatia mifumo, misingi na kanuni za kimataifa iliyowekwa kwa lengo la kuimarisha amani na usalama.

Sauti
3'5"
Katibu Mkuu wa UM Antonio Guterres akiwa na Mwenyekiti wa tume ya Muungano wa Afrika, AU Moussa Faki Mahamat kwenye mkutano na wanahabari jijini New York Marekani.
PICHA: UN /Manuel Elias

UN na AU zafuatilia hali ya kisiasa Guinea- Bissau

Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres na mwenyekiti wa Tume ya Umoja wa Afrika Moussa Faki Mahamat wameendelea kuwa na  wasiwasi juu ya mgogoro wa kisiasa wa muda mrefu nchini Guinea-Bissau licha ya jitihada za  jamii ya kimataifa za kujaribu mbinu za upatanisho baina ya vyama vya kisasa nchini humo.