Umoja wa Mataifa, UN na Muungano wa Afrika, AU wameelezea wasiwasi wao mkubwa juu ya sintofahamu inayoendelea kukumba mfumo wa dunia na kusababisha madhara kwenye amani na usalama duniani.
Katibu Mkuu wa UN Antonio Guterres na Mwenyekiti wa kamisheni ya AU Moussa Faki Mahamat wamesema hayo katika taarifa yao ya pamoja waliyoitoa mwishoni mwa mkutano wa pili wa kila mwaka wa vyombo hivyo viwili mjini Addis Ababa nchini Ethiopia hii leo.
Wamesema kila nchi inapaswa kuzingatia mifumo, misingi na kanuni za kimataifa iliyowekwa kwa lengo la kuimarisha amani na usalama.