Watoto wachanga 11 wateketea baada ya wodi ya wazazi kuungua Senegal:UNICEF
Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF limeeleza kusikitishwa na vifo vya takriban watoto 11 wachanga waliozaliwa hivi karibuni, kufuatia moto katika kitengo cha watoto wachanga cha hospitali ya Tivaouane nchini Senegal.