Skip to main content

Chuja:

Monduli

17 JULAI 2023

Hii leo katika jarida la Habar iza UN, mwenyeji wako Leah Mushi anamulika haki za binadamu za watu wa jamii ya asili, haki ya elimu kwa watoto wakimbizi, saratani ya shingo ya kizazi na hatimaye jinsi kampeni ya boma kwa boma inasongesha utoaji chanjo kwa jamii ya wamasai nchini Tanzania.

Sauti
11'11"
Wanawake wa Kimaasai Monduli nchini Tanzania wageukia ufugaji nyuki ili kujikwamua kiuchumi.
FAO Tanzania

Wanawake wa kimaasai Monduli wageukia ufugaji nyuki kwa hisani ya FAO na wadau

Kaskazini mwa Tanzania, ukame wa mara kwa mara katika miaka ya hivi karibuni umeweka shinikizo kwa jamii zilizozooea kujipatia riziki kwa kufuga ng'ombe. Kundi la wanawake wa Kimasai wamegeukia kuzalisha asali kutoka kwenye mizinga ya nyuki msituni ili kujipatia kipato cha ziada. Hii imehakikishia mustakabali wa watoto wao na inasaidia kuzalisha upya msitu unaozunguka mizinga yao.

Pale Mmaasai mwanaume anapopigia chepuo haki za wamasai wanawake

Ni kawaida kwa mtu anayeamua kusimama kidete dhidi ya mila zinazopigiwa chepuo na wenzake kukumbwa na misukosuko! Na ni misukosuko zaidi pindi mtu huyo ni wa kabila la kimasai na ni mwanaume anayetetea haki za wamasai wanawake na wasichana wanaokumbana na mila potofu kama vile ukeketeji na kupokwa ardhi zao pindi mume anapofariki dunia. Hivyo ndivyo ilivyokuwa kwa Alais Esoto, mratibu wa shirika la kiraia la Naserian huko Monduli mkoani Arusha nchini Tanzania. Alikumbana na mengi lakini hakukata tamaa na sasa ameona matunda.

Sauti
4'22"
UN News/Assumpta Massoi

Elimu ndio mkombozi wa msichana wa kimasai

Ukosefu wa usawa kati ya maeneo ya mijini na vijijini ni kikwazo kwa maendeleo ya jamii. Na tofauti hiyo inazidi zaidi pindi jamii hiyo ina wanawake ambao kwao mahitaji yao yanapuuzwa licha ya kwamba wana mchango mkubwa katika maendeleo ya jamii zao. Kutoka Arusha Tanzania, Assumpta Massoi amezungumza na Maria Mamasita mshiriki wa mkutano wa 62 wa kamisheni ya hali ya wanawake duniani, CSW62 ulioanza tarehe 12 mwezi huu wa Machi, mada kuu ikiangazia kumwendeleza mwanamke wa kijijini. Je wao wanafanya nini?

Sauti
2'8"
UN News/Assumpta Massoi

Elimu ni mkombozi kwa msichana wa kimasai- Mamasita

Mkutano wa 62 wa Kamisheni ya Hali ya wanawake duniani, CSW62 umeanza makao makuu ya Umoja wa Mataifa, kubwa zaidi linaloangaziwa ni wanawake na wasichana wa vijiji. Wawakilishi wa mashirika ya kiraia wamefika na miongoni mwao ni Maria Mamasita kutoka Monduli mkoa wa Arusha nchini Tanzania.

Sauti
2'8"
Uwezeshaji wanawake na wasichana ndio muarobaini wa kufanikisha ajenda ya 2030. Pichanini Juba huko Sudan Kusini wanawake wakiwa kwenye maandamano.
UN /JC McIlwaine

Kubadili maisha yako yahitaji kubadili mtazamo wako- Terry

Mkutano wa 62 wa kamisheni ya hali ya wanawake, CSW62 uking'oa nanga hii leo, washiriki nao wanapaza sauti ni kipi wanafanya kubadili maisha ya wanawake wa vijijini. Leo tumezungumza na washiriki kutoka Monduli mkoani Arusha nchini Tanzania pamoja na kutoka kaunti ya Kwale huko Mombasa nchini  Kenya.