Chuja:

Mombasa

UN News

Mradi wa PLEAD wawezesha huduma za mahamaka kupatikana muda wote nchini Kenya

Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya madawa na uhalifu UNDOC kanda ya Afrika Mashariki kwa kushirikiana na sekta ya mahakama nchini kenya wamepanga kuanza kutekeleza awamu ya pili ya mradi wa uwekaji umeme wa sola katika mahakama na magereza nchini humo baada ya awamu ya kwanza kuonesha mafanikio.

Kupitia mradi ujulikanao kama PLEAD unaofadhiliwa na Muungano wa Ulaya UNODC na sekta ya mahakama nchini Kenya wamefanikiwa kutekeleza mradi wa awamu ya kwanza katika mahakama mbili zilizoko Mombasa ambazo zilikuwa zikishindwa kuendesha shughuli zake pindi umeme unapokatika.

Sauti
3'23"

24 Julai 2019

Katika Jarida la Habari hii leo arnold Kayanda anakuletea 

-Mikoko yaleta nuru kwa wakazi wa Pwani ya kenya licha ya kuhifadhi mazingira kwa kupunguza hewa ukaa yawaletea kipato wananchi kwa mujibu wa UN Environment

-Vijana nchini Tanzania wakumbatia mabadiliko ya kuachana na matumizi ya mifuko ya plastiki na kujipatia kipato kwa kutengeneza mifuko mbadala ya karatasi

-Elimu katika shule 25 nchini Kenya yapigwa jeki na mradi wa UNICEF wa  vitabu mtandaoni na matumizi ya Ipad

Sauti
13'35"
UN-Habitat/Julius Mwelu

Haki Afrika yaenda maskani kukutana na vijana

Nchini Kenya, shirika la kiraia la Haki Afrika limechukua hatua ya kufuata vijana maskani kama njia mojawapo ya kufanikisha utekelezaji wa lengo namba 16 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs.

Afisa mradi wa Haki Afrika, Wevyn Muganda amesema hayo akihojiwa na Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani baada ya kuhutubia Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuhusu amani na usalama na jinsi ya utekelezaji wa ajenda ya vijana na amani.

Sauti
2'46"
UN News/Patrick Newman

COVAW yabadili maisha ya wasichana wa kaunti ya Kwale

Utalii wasifika sana kwa kuinua kipato cha nchi ya Kenya iliyoko Afrika Mashariki. Hata hivyo baadhi ya watalii wawe wa ndani au wa nje wanatumia fursa hiyo kutekeleza mambo yanayokiuka haki za binadamu hususan kufanya biashara ya ngono. Kutokana na umaskini baadhi ya wasichana kwenye kaunti ya Kwale huko Mombasa, wametumbukia katika mtego wa biashara ya ngono au hata biashara ya binadamu na kujikuta na madhila makubwa zaidi. Shirika moja la kiraia linalopinga ukatili na ghasia dhidi ya wanawake nchini Kenya, COVAW limechukua hatua. Je ni hatua gani?

Sauti
3'53"