Shambulizi la kujitoa muhanga Somalia, Umoja wa Mataifa walaani
Stéphane Dujarric ambaye ni Msemaji wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa hii leo akizungumza na waandishi wa habari katika makao makuu ya UN amesema Shirika hilo linalaani shambulizi la kujitoa muhanga lilitokea leo katika mji mkuu wa Somalia, Mogadishu, akiongeza kusema, tunatoa "rambirambi zetu kwa familia za waathiriwa," na akawatakia ahueni ya haraka wale wote waliojeruhiwa.