Ni wakati wa hatua za mageuzi kuhusu ubinadamu- Ban
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki-moon, amesema sasa ndio wakati wa kuchukua hatua madhubuti kwa minajili ya kushughulikia mahitaji makubwa ya kibinadamu, na kwamba dunia sasa hivi inakabiliwa na changamoto ya aina yake.
Ban amesema hayo katika taarifa iliyochapishwa leo kwenye tahariri ya gazeti la The Guardian, ambapo ameandika kuwa watu milioni 130 kote duniani wanahitaji usaidizi wa kibinadamu, wakati watu zaidi ya milioni 60 wakiwa wamelazimika kuhama makwao.
Tumbuizo katika mkutano wa utu wa kibinadamu #WHS
"Mtazamo wa uhamiaji na wahamiaji unachukuliwa kama kitu kibaya". Hiyo ni kauli ya mkurugenzi mkuu wa Shirika la uahamiaji duniani IOM William Swing alipohutubia mkutano wa utu wa kibindamu uliofanyika Mei 23 hadi 24 mjini Istanbul Uturuki. Bw. Swing anasema kwamba ni lazima mtazamo huo ubadilidhwe ikizingatiwa kwamba nchi nyingi zimejengwa kwa nguvu za wahamiaji na kwamba uhamiaji ni kitu kizuri na ni vyema kurejelea dhana hiyo.
#WHS: Wanawake wapewe kipaumbele katika kushughukilia masuala ya kibinadamu
Kila kunapozuka dharura katika jamii waathirika wakubwa ni wanawake ingawa jamii nzima inaathirika. Hivyo wito umetolewa wa kuwapa kipaumbele wanawake hasa zahma za kijamii zinapotokea.
Wito huo umetolewa na mwakilishi wa vijana wa shirika la Umoja wa mataifa la kuhudumia watoto UNICEF nchini Kenya Hanna Wanja Maina akiwa mjini Istanbul Uturiki wakati wa hitimisho la mkutano wa dunia wa masuala ya kibinadamu alipozungumza na Radio ya Umoja wa mataifa
(HANNA 1).
Hanna anaeleza pia nini amejifunza kwenye kongamano hilo la kimataifa
(HANNA 2)
#WHS yaridhia hati ya kulinda maslahi ya watu wenye ulemavu
Pamoja na mambo mengine hati hiyo inasihi serikali na mashirika ya kiraia sambamba na wahisani kuhakikisha hatua zote za kibinadamu wakati wa majanga zinakidhi misingi mitano.
Misingi hiyo ni pamoja na kutobagua na kutambua aina mbali mbali za ulemavu wakati wa majanga, kushirikisha watu wenye ulemavu katika mipango ya usaidizi wa kibinadamu, kuhakikisha mipango yote ya usaidizi inafikishiwa watu wote wenye ulemavu na kutekeleza sera shirikishi.
Boko Haramu inaendelea kuwaweka roho juu wananchi Nigeria:WHS
Kundi la Boko Haramu ambalo linalaumiwa kwa ukatili, mauaji na vitendo vya kigaidi linaendelea kuziweka jamii roho juu katika maeneo mbalimbali nchini Nigeria likiwemo jimbo la Adamawa Kaskazini Mashariki mwa Nigeria ambako watu wanafungasha virago kila uchao kwa sababu ya kundi hilo.
Aishatu Marginal mwenye umri wa miaka 59, ni muuguzi mstaafu,amekuwa Istanbul Uturuki kwenye mkutano wa dunia wa masuala ya kibinadamu kuwakilisha jamii iliyoathirika na Boko Haramu.
Binafsi amesaidia kuwapa hifadhi zaidi ya wakimbizi wa ndani 50 kwa muda wa miezi saba. Ilikuwaje?