Ni wakati wa hatua za mageuzi kuhusu ubinadamu- Ban
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki-moon, amesema sasa ndio wakati wa kuchukua hatua madhubuti kwa minajili ya kushughulikia mahitaji makubwa ya kibinadamu, na kwamba dunia sasa hivi inakabiliwa na changamoto ya aina yake.
Ban amesema hayo katika taarifa iliyochapishwa leo kwenye tahariri ya gazeti la The Guardian, ambapo ameandika kuwa watu milioni 130 kote duniani wanahitaji usaidizi wa kibinadamu, wakati watu zaidi ya milioni 60 wakiwa wamelazimika kuhama makwao.