Tanzania na mpango shiriki wa uhifadhi wa misitu
Ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa kuhusu hali ya misitu duniani imezitaka serikali kuchukua hatua jumuishi katika ulinzi na uhifadhi wa misitu ili kupunguza kasi ya kupungua kwa eneo la misitu kila uchao.
Kwa mujibu wa shirika la chakula na kilimo duniani, FAO ambalo ndio mwandishi wa ripoti hiyo, hatua kama vile kupunguza ukataji miti holela, matumizi endelevu ya misitu na kupanda miti ni hatua ambazo zinapaswa kutekelezwa kwa kutumia jamii zinazonufaika na rasilimali za misitu.