Skip to main content

Chuja:

misitu

UNMISS/Eric Kanalstein

Tanzania na mpango shiriki wa uhifadhi wa misitu

Ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa kuhusu hali ya misitu duniani imezitaka serikali kuchukua hatua jumuishi katika ulinzi na uhifadhi wa misitu ili kupunguza kasi ya kupungua kwa eneo la misitu kila uchao. 

Kwa mujibu wa shirika la chakula na kilimo duniani, FAO ambalo ndio mwandishi wa ripoti hiyo, hatua kama vile kupunguza ukataji miti holela, matumizi endelevu ya misitu na kupanda miti ni hatua ambazo zinapaswa kutekelezwa kwa kutumia jamii zinazonufaika na rasilimali za misitu.

Sauti
1'47"

Je Tanzania ya kijani inawezekana? Dk Mwakaluka

Umoja wa Mataifa na wadau mbalimbali wamekuwa mstari wa mbele katika uhifadhi wa mazingira ili kubabiliana na tatizo la  tabianchi. Kampeni moja wapo katika ulinzi wa mazingira ni uhifadhi wa misitu ya asili na pia upandaji miti ili kufukia lengo la Umoja wa Mataifa la kuongeza misitu yote ya dunia  kwa asilimia  3 ifikapo mwaka 2030.

Sauti
3'59"

Mbadala wa kuni na mkaa utamrahisishia kazi mwanamke na kulinda misitu:Buhero

Matumizi ya nishati haribifu kwa misitu na mazingira kama kuni na mkaa kwa kiasi kikubwa yakimuhusisha mwanamke yanahitaji nishati mbadala na hususani kwa nchi zinazoendelea ambako asilimia kubwa ya watu wanaishi vijijini na hawana fursa ya kupata nishati nyingine kwa matumizi ya kawaida. Serikali ya Tanzania imetambua hilo na kwa kushirikiana na wadau mbalimbali likiwemo shirika la umoja wa Mataifa la mazingira UNEP na makampuni binafsi wanaihamasisha jamii kuingia katika matumizi ya gesi.

Sauti
4'16"