Zaidi ya nchi 100 zimeahidi kusitisha na kubadilisha ukataji miti ifikapo 2030
Azimio la kihistoria la kuokoa na kurejesha misitu ya dunia katika ubora wake limetangazwa leo rasmi katika siku ya pili ya mkutano wa Umoja wa Mataifa wa mabadiliko ya tabianchi unaoshirikisha viongozi wa dunia au COP26.