Skip to main content

Chuja:

misitu

©FAO/Xiaofen Yuan

Nguvu ya mwanamke yaokoa msitu wa Imacata nchini Venezuela

Wanawake wa jamii ya asili katikati ya msitu wa hifadhi wa Imacata nchini Venezuela wamechukua jukumu la kulinda ardhi yao iliyoathiriwa kwa miaka mingi kutokana na shughuli za madini na ukataji miti. Shirika la Umoja wa Mataifa la kilimo na chakula FAO limeunga mkono juhudi za wanajamiii hao kwa kutoa miche ya kurejesha uoto wa asili. Grace Kaneiya anataarifa zaidi.

(Taarifa ya Grace Kaneiya)

Sauti
2'55"
UN News/ John Kibego

Ugunduzi wa rasilimali ya mafuta huwa ni wa kujivunia lakini unakuja na changamoto zake

Ugunduzi wa rasilimali ya mafuta hua ni wa kujivunia kwani huleta fursa nyingi zikwemo ajira, ukwaji wa miji, viwanda na hata uchumi wa taifa kwa ujumla.

Lakini kwa upande mwingine hua na madhara kwa mazingira na jamii ambayo huathiri zaidi watu wa kipato cha chini katika jamii husika.

Uganda inajiandaa kuanza kuzalisha mafuta katika eneo la Bonde la Ufa la Ziwa Albert ambapo sasa wanamazingira wanaonya kuhusu athari za viwanda vya mafuta wakati ambapo misitu ya asili inazidi kuchafuliwa kwa ajili ya kilimo na makaazi.

Je, wanasema ini?

Sauti
3'50"
FAO/Rudolf Hahn

Ripoti ya FAO yaonesha dunia imepoteza ekari milioni 178 za misitu tangu 1990

Ripoti mpya ya tathimini ya rasilimali ya misitu iliyotolewa na shirika la Umoja wa Mataifa la kilimo na chakula FAO imesema upotevu wa misitu duniani bado unaendelea ingawa sio kwa kiwango kikubwa sana. Jason Nyakundi anaarifu zaidi.

Ripoti hiyo mpya ya aina yake iliyozinduliwa leo mjini Roma Italia kwa mujibu wa FAO ni ya kina na imemulika zaidi ya vyanzo 60 vya upotevu wa misitu kwa kipindi cha kuanzia mwaka 1990 hadi 2020.

Sauti
5'49"

21 JULAI 2020

Katika Jarida la Habari za Umoja wa Mataifa hii leo Flora Nducha anakuletea

- Shirika la Umoja wa Mataifa la chakula na kilimo FAO limetoa ripoti mpya ya tathimini ya misitu duniani ikionyesha kwamba misitu inaendelea kupotea kutokana na matumizi mbalimbali ikiwemo kilimo na upanuzi wa makazi hasa barani Afrika

-Vijana watatu nchini Tanzania wamebuni mfumo wa kuweka umeme kwenye mita kwa njia ya simu ambao utawasahisishia wateja wa huduma hiyo muhimu

Sauti
11'24"