Baraza Kuu la UN lakamilisha mkutano wa 72
Mkutano wa 72 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa umetamatishwa hii leo ambapo aliyekuwa rais wake Miroslav Lajčák ametaja mambo sita muhimu aliyobaini wakati wa uongozi wake tangu mwezi Septemba mwaka jana.
Mkutano wa 72 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa umetamatishwa hii leo ambapo aliyekuwa rais wake Miroslav Lajčák ametaja mambo sita muhimu aliyobaini wakati wa uongozi wake tangu mwezi Septemba mwaka jana.
Mkutano wa 72 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa umetamatishwa hii leo ambapo aliyekuwa rais wake Miroslav Lajčák ametaja mambo sita muhimu aliyobaini wakati wa uongozi wake tangu mwezi Septemba mwaka jana.
Hoja za nini kifanyike ili kuepusha mizozo na badala yake kuweka mazingira ya ujenzi wa amani endelevu zimewasilishwa hii leo kwenye Umoja wa Mataifa wakati wa kikao cha ngazi ya juu kilichoandaliwa na Baraza Kuu la umoja huo.
Viongozi wa ngazi ya juu wakiwemo marais, wafalme, mawaziri wakuu na viongozi waandamizi wa nchi wanachama wametoa mitazam yao wakati huu ambapo Umoja wa Mataifa unasema kila kona mizozo inachipua na kule ambako ilishaanza inaota mizizi.
Masuala ya amani na usalama ni muhimu mno kwa ajili ya maendeleo na suluhu ya pamoja. Kwa muktada huo Umoja wa Mataifa utajadili kwa kina masuala hayo kuanzia kesho Jumanne kwenye mkutano utakaofanyika makao makuu ya Umoja huo mjini New York Marekani.
Rais wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa Miroslav Lajčák amefungua jukwaa la watu wa jamii ya asili akisema katu isisahaulike kuwa Umoja wa Mataifa ni kwa ajili ya watu wote ikiwemo watu wa asili.
Amewaambia wajumbe kuwa ingawa kuna mafanikio yamepatikana katika kujumuisha kundi hilo bado juhudi zinatakiwa ikiwemo kuwanasua katika lindi la umaskini.
Amesema asilimia 15 ya watu wote maskini duniani ni watu wa jamii ya asili .
(Sauti ya Miroslav Lajčák )
Rais wa baraza kuu la Umoja wa Mataifa, Bwana Miroslav Lajčák, amehitimisha ziara yake ya siku mbili nchini Colombia ambako alikutana na vyongozi wa ngazi ya juu serikalini na asasi za kiraia ili kuzungumzia azma ya utekelezaji wa amani na maendeleo andelevu SDGs.
Rais wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa Miroslav Lajčák aliyeko ziarani nchini Kenya, amesema maendeleo hayapaswi kusababisha uharibifu wa mazingira.
Amesema hayo jijini Nairobi, wakati akifunga mjadala kuhusu sayansi, sera na biashara, mjadala uliofanyika kwa siku mbili.
Bwana Lajčák amesema hayo akizingatia kuwa harakati za sasa za maendeleo duniani zimekumbwa na vikwazo kama vile majanga ya asili na yale yanayosabishwa na binadamu ambavyo vyote vinatishia siyo tu uwepo wa binadamu bali pia sayari dunia.