Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Miroslav Lajčák

Picha na UN/Staton Winter

Amani si bidhaa unatengeneza na kuuza

Hoja za nini kifanyike ili kuepusha mizozo na badala yake kuweka mazingira ya ujenzi wa amani endelevu zimewasilishwa hii leo kwenye Umoja wa Mataifa wakati wa kikao cha ngazi ya juu kilichoandaliwa na Baraza Kuu la umoja huo.

 

Viongozi wa ngazi ya juu wakiwemo marais, wafalme, mawaziri wakuu na viongozi waandamizi wa nchi wanachama wametoa mitazam yao wakati huu ambapo Umoja wa Mataifa unasema kila kona mizozo inachipua na kule ambako ilishaanza inaota mizizi.

 

Sauti
1'35"
Miroslav Lajčák rais wqa baraka za kuu la Umoja wa Mataifa
Picha ya UM/Evan Schneider

Amani ndio muhimili wa kila kitu: LAJCAK

Masuala ya amani na usalama  ni muhimu mno kwa ajili ya maendeleo na suluhu ya pamoja. Kwa muktada huo Umoja wa Mataifa utajadili kwa kina masuala hayo kuanzia kesho Jumanne kwenye mkutano utakaofanyika makao makuu ya Umoja huo mjini New York Marekani.

Sauti
1'25"
UN / Evan Schneider

Ardhi zao zinaporwa, mifumo ya kuwalinda inawaengua

Rais wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa Miroslav Lajčák amefungua jukwaa la watu wa jamii ya asili akisema katu isisahaulike kuwa Umoja wa Mataifa ni kwa ajili ya watu wote ikiwemo watu wa asili.

Amewaambia wajumbe kuwa ingawa kuna mafanikio yamepatikana katika kujumuisha kundi hilo bado juhudi zinatakiwa ikiwemo kuwanasua katika lindi la umaskini.

Amesema asilimia 15 ya watu wote maskini duniani ni watu wa jamii ya asili .

(Sauti ya Miroslav Lajčák )

Sauti
1'48"

Tuwe makini maendeleo yasisababishe zahma- Lajčák

Rais wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa Miroslav Lajčák aliyeko ziarani nchini Kenya, amesema maendeleo hayapaswi kusababisha uharibifu wa mazingira.

Amesema hayo jijini Nairobi, wakati akifunga mjadala kuhusu sayansi, sera na biashara, mjadala uliofanyika kwa siku mbili.

Bwana Lajčák amesema hayo akizingatia kuwa harakati za sasa za maendeleo duniani zimekumbwa na vikwazo kama vile majanga ya asili na yale yanayosabishwa na binadamu ambavyo vyote vinatishia siyo tu uwepo wa binadamu bali pia sayari dunia.