Chuja:

Millie Bobby Brown

Rangi ya buluu iliangaza ndani ya ukumbi wakati wa maadhimisho ya miaka 30 ya mkataba wa kimataifa wa haki za mtoto, CRC.
UN Photo/Manuel Elías

Rangi ya buluu ikitawala, Beckham asema "siku zijazo ni za watoto wetu hivyo tutunze ndoto zao"

Mustakabali si wa kwetu bali ni wa watoto wetu kwa hiyo tuchukue hatua zaidi kulinda ndoto za watoto, amesema David Beckham, Balozi mwema wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF, wakati akihutubia hii leo kikao cha ngazi  ya  juu cha Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani kilichofanyika kuadhimisha miaka 30 tangu kupitishwa kwa mkataba wa haki za mtoto, CRC na sambamba na siku ya mtoto duniani,

 

Millie Bobby Brown akiwa mjini New York wakati wa kutengeneza video ya siku ya mtoto mwaka 2018
UNICEF/UN0248272/Clarke

Leo ni siku kubwa kwa watoto kote duniani.

Wakati dunia ikiadhimisha siku ya mtoto duniani, Millie Bobby Brown ametangazwa kuwa balozi mwema mpya wa Shirika la kuhudumia watoto UNICEF.  Mtoto huyu wa umri wa miaka 14 anakuwa mtu mdogo zaidi kuwa na wadhifa huo wa balozi mwema wa UNICEF.