Skip to main content

Chuja:

Mikoko

26 JULAI 2022

Hii leo jaridani Anold Kayanda anakuletea Habari kwa Ufupi; Mada Kwa Kina na Mashiani:

Katika Mada kwa Kina anasalia makao makuu ya Umoja wa Mataifa ambako wiki iliyopita Naibu Katibu Mkuu wa  Umoja wa Mataifa Amina J, Mohammed alizindua maonesho ya “Ulikuwa umevaa nini? Yakionesha nguo ambazo walivalia manusura wa ukatili wa kingono, kwa kuzingatia kuwa jamii humbebesha lawama ya kubakwa yule aliyebakwa badala ya aliyebakwa kwa kisingizio cha mavazi.

Sauti
12'24"
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres (katikati) akutana na wanachama wa vyama vya ushirika vya kilimo vinavyoongozwa na wanawake na wanaume wazawa katika Kijiji cha Pierre Kondre-Redi Doti, katika ukanda wa msitu wa kitropiki wa Suriname.
UN Photo/Evan Schneider

Suriname inatoa “tumaini na msukumo kwa ulimwengu kuokoa misitu yetu ya mvua”: Mkuu wa UN

Suriname inaweza kuwa nchi ndogo na isiyo na watu wengi zaidi katika ukanda wa  Amerika ya Kusini, lakini ni moja ya nchi za kijani kibichi. Inachukuliwa kuwa kinara wa kimataifa katika uhifadhi wa bioanuwai, huku zaidi ya asilimia 90 ya ardhi yake ikifunikwa na misitu ya asili, rasilimali asilia isiyo na kifani ya taifa zaidi ya kufidia saizi yake.

Maktaba

Utunzaji wa mikoko wainua kipato cha wavuvi

Nchini Senegal, mradi wa pamoja wa mfuko wa Umoja wa Mataifa wa maendeleo ya kilimo duniani, IFAD na serikali ya taifa hilo la Afrika Magharibi umesaidia kurejeshwa upya kwa maelfu ya hekta za mikoko baharini na hivyo kusaidia jamii za wavuvi kuinua kipato chao na wakati huo huo kuwa na  mnepo dhidi ya mabadiliko ya tabianchi. 

Sauti
3'6"

Jarida 15 Septemba 2021

Katika jarida hii leo utasikia jukwaa maalum lililoanzishwa na shirika la afya la Umoja wa Mataifa WHO kwa ajili ya elimu ya kung'atwa na nyoka. Nchini Senegal mradi wa kunusuru mikoko umesaidia wavuvi kuongeza kipato na nchini Afghanistan ndege za misaada zaanza kushusha chakula na vifaa vya matibabu. 

Ungana na Assumpta Massoi kwa undani wa taarifa hizo.

Sauti
14'27"
Mikoko inasadia kutunz mazingira ambayo husaidia mazao ya baharini kuwa na faida
Manglar Vivo Project, UNDP Cuba

Mradi wa kuhifadhi mikoko Senegal waongeza pia kipato cha wavuvi wa chaza

Nchini Senegal, mradi wa pamoja wa mfuko wa Umoja wa Mataifa wa maendeleo ya kilimo duniani, IFAD na serikali ya taifa hilo la Afrika Magharibi umesaidia kurejeshwa upya kwa maelfu ya hekta za mikoko baharini na hivyo kusaidia jamii za wavuvi kuinua kipato chao na wakati huo huo kuwa na  mnepo dhidi ya mabadiliko ya tabianchi.

Sauti
3'6"
mtoto Mwigulu Matonange Magesa mwenye umri wa miaka 16 kutoka Tanzania anayeishi na ualbino.
UN News/Video capture

Iwapo ulizikosa wiki hii ya 22-26 Julai 2019

Mkurugenzi Mkuu wa shirika la nishati ya atomiki duniani, IAEA, Yukia Amano, aaga dunia, siku chache tu kabla ya kuwasilisha barua yake ya kujiuzulu wadhifa huo. Suala la wahamiaji na wakimbizi wanaosaka maisha bora barani Ulaya kupitia Mediteranea lapigiwa chepuo kwa hatua mpya chanya barani humo. Nchini Kenya mradi mpya kwenye pwani ya nchi hiyo washamirisha mikoko na biashara ya hewa ya ukaa. Baa la nzige latishia mustakabali wa chakula kwenye pembe ya Afrika na Yemen, na mtoto Mwigulu ambaye alikatwa mkono kisa tu ni albino azungumza na Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa.