Baraza kuu la UNHABITAT laanza Nairobi likijikita na miji endelevu kwa ajili ya kutimiza SDGs
Mkutano wa pili wa Baraza Kuu la shirika la Umoja wa Mataifa la makazi UNHABITAT umeanza leo mjini Nairobi Kenya ukibeba maudhui “Mustakabali endelevu wa miji kupitia ujumuishwaji na na ufanisi wa ushirikiano wa kimataifa: kufikia Malengo ya Maendeleo Endelevu wakati wa majanga ya kimataifa.”