FAO yatumia msemo wa tahadhari kabla ya hatari kunusuru mali na uhai Bangladesh
Nchini Bangladesh, shirika la Umoja wa Mataifa la chakula na kilimo, FAO limechukua hatua kusaidia wakulima na wafugaji kuepuka madhara makubwa ya majanga ya kiasili kama vile mafuriko ambayo yamekuwa yanakumba mara kwa mara taifa hilo na kusababisha wakulima na wafugaji kupoteza siyo tu mifugo yao bali pia chakula cha mifugo, mazao na makazi yao na hivyo kuwaacha katika lindi la umaskini.