Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

mifugo

Chakula kwa ajili ya mifugo kilichotengenezwa kutokana na soya, moja ya bidhaa kubwa zinazosafirishwa kutoka Amerika ya kusini, kinaaongoza kwa ukataji mkubwa wa miti na kuwaondoa wakulima na wakazi wa asili katika maenewo yao duniani kote
FAO/Carly Learson

FAO yatumia msemo wa tahadhari kabla ya hatari kunusuru mali na uhai Bangladesh 

Nchini Bangladesh, shirika la Umoja wa Mataifa la chakula na kilimo, FAO limechukua hatua kusaidia wakulima na wafugaji kuepuka madhara makubwa ya majanga ya kiasili kama vile mafuriko ambayo yamekuwa yanakumba mara kwa mara taifa hilo na kusababisha wakulima na wafugaji kupoteza siyo tu mifugo yao bali pia chakula cha mifugo, mazao na makazi yao na hivyo kuwaacha katika lindi la umaskini.

Sauti
2'41"
WFP/Peter Louis

Kama nzige hawa hawataisha na mvua ikanyesha japo kiasi, mifugo yetu itakufa- Wafugaji Turkana

Hivi karibuni tulikueleza namna ambavyo nzige wavamizi wa jangwani wanavyotishia ustawi wa wakulima wa Kenya hususani eneo katka eneo la Turkana, lakini kwa mujibu wa shirika la chakula na kilimo la Umoja wa mataifa FAO, nzige hao hawaishii tu katika kilimo bali pia wanatishia jamii ya wafugaji kwani wanakula hadi nyasi na miti amayo ingekuwa chakula cha kifugo. John Kibego na maelezo zaidi. 

Sauti
2'50"

16 JANUARI 2020

Katika Jarifada la Habari la Umoja wa Mataifa hii leo Grace Kaneiya anakuletea

-Watu milioni 45 katika nchi 16 za Kusini mwa Afrika maisha yao yako hatarini kutokana na njaa, na hatua za haraka za msaada zinahitajika limesema shirika la Umoja wa Matafa la mpango wa chakula duniani WFP

-Kimbunga Idai kilifungua macho ya madhila yanayowasibu watu wenye ulemavu nchini Zimbawe kwa mujibu wa shirika la Umoja wa Mataifa la elimu , sayansi na elimu, UNESCO

Sauti
11'44"
Sehemu ya madhara ya kimbunga Idai katika eneo la bandari ya Beira nchini Msumbiji.
WFP/Maktaba

IAEA yaisaidia Msumbiji kukabiliana na maradhi ya mifugo baada ya mafuriko:

Shirika la kimataifa la nguvu za atomiki IAEA, limepeleka vifaa vya dharura ili kuisaidia Msumbiji kupambana na mgonjwa ya mifugo kama homa ya Afrika ya nguruwe, ugonjwa wa miguu na midomo  au homa ya bonde la ufa magonjwa ambayo yanaweza kuleta athari kubwa na kutishia mustakabali wa mifugo na binadamu baada ya mafuriko yaliyosababishwa na vimbunga vya hivi karibuni.

27 Juni 2019

Miongoni mwa habari anazokuletea hii leo arnold Kayanda katika Jarida laletu ni pamoja na 

-Halahala yatolewa na shirika la afya ulimwenguni watu kupata chanjo ya surua kabla ya kwenda nchi zenye mlipuko wa ugonjwa huo

-Nchini Mali tunamulika masuala ya ukwepaji sheria dhidi ya wanaoshambulia raia , uchunguzi ukifanyika chini ya mpango wa umoja wa Mataifa MINUSMA

-Madhila anayosimulia mkimbizi toka Yemeni kuwa kila anakokimbilia na wanawe, ni kaburi tu

- Makala yetu leo inatupeleka Uganda ambako chepuo yapigwa kutika mazingira ili kuepuka maafa ya mifugo

Audio Duration
12'43"