Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

mifugo

Mifugo ni uti wa mgongo wa uchumi vijijini wa Sudan, unaowapa mamilioni ya watu usalama wa chakula na lishe, kipato, na maisha bora.
© FAO/Antonello Proto

FAO yaanza kampeni ya chanjo ya mifugo milioni 9.4 kote nchini Sudan

Shirika la Umoja wa Mataifa la  Chakula na Kilimo  Duniani (FAO), kwa kushirikiana na Serikali ya Sudan, limezindua kampeni ya kitaifa ya chanjo ya mifugo kwa mwaka 2025 ili kulinda maisha na riziki za  wafugaji na wakulima wanaokadiriwa kuwa zaidi ya milioni tatu kote nchini Sudan, ambao wanakabiliwa na janga kubwa la uhaba wa chakula.

Kliniki pekee ya mifugo huko Bor, Sudan Kusini, inayosimamiwa na daktari wa UNMISS kutoka Jeshi la India.
UNMISS

FAO yatoa ramani mpya ya usambazaji wa mbu wa Tse Tse barani Afrika

Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo (FAO) limezindua ramani mpya ya usambazaji wa mbu wa tse tse barani Afrika, zana muhimu katika vita dhidi ya ugonjwa wa trypanosomosis unaoathiri mifugo na kusababisha hasara kubwa kwa wakulima kusini mwa Jangwa la Sahara. Ramani hii imekusudiwa kuwa msingi wa kisayansi katika kudhibiti ugonjwa huo ambao unasababisha madhara makubwa ya kiuchumi kwa mifugo barani Afrika.

05 JULAI 2024

Hii leo kwenye jarida mwenyeji wako ni Assumpta Massoi akimulika shamrashamra za Kiswahili, wakimbizi na wahamiaji na mateso njiani Afrika, mafunzo kwa wataalamu wa mifugo Tanzania na harakati za OCHA Sudan kusaidia wahitaji.

Sauti
9'49"
UN News

FAO Tanzania na USAID wafanikisha mafunzo kwa Maafisa Mifugo Tanzania

Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo (FAO) kwa ufadhili ya Shirika la Marekani la misaada ya maendeleo (USAID), limehitimisha awamu ya nne ya mafunzo kwa Maafisa Mifugo 30 wa serikali ya Tanzania, yatakayowawezesha kutambua na kutibu magonjwa ya mifugo ili kuboresha ufugaji wenye tija na kulinda soko la Mifugo kimataifa. Hamad Rashid wa Redio washirika MVIWATA FM ya Morogoro, amehudhuria shughuli ya uhitimishaji wa mafunzo hayo na kuandaa makala inayoanza na ujumbe wa Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Tanzania, Profesa Riziki Shemdoe.

Sauti
3'15"
UN News

FAO yaimarisha Afya ya Mifugo Kupitia mradi wa ISAVET nchini Tanzania

Nchini Tanzania, Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO) linaendesha programu ya mafunzo yanayolenga kuboresha ujuzi wa wataalamu wa mifugo katika kudhibiti magonjwa ya wanyama na kuimarisha afya ya mifugo ili kuihakikishia jamii uhakika wa chakula na chakula salama. John Kabambala wa redio washirika wetu KidsTime ya mkoani Morogoro Tanzania amezungumza na wadau kandoni mwa mafunzo hayo. 

Sauti
5'8"
Chakula kwa ajili ya mifugo kilichotengenezwa kutokana na soya, moja ya bidhaa kubwa zinazosafirishwa kutoka Amerika ya kusini, kinaaongoza kwa ukataji mkubwa wa miti na kuwaondoa wakulima na wakazi wa asili katika maenewo yao duniani kote
FAO/Carly Learson

FAO yatumia msemo wa tahadhari kabla ya hatari kunusuru mali na uhai Bangladesh 

Nchini Bangladesh, shirika la Umoja wa Mataifa la chakula na kilimo, FAO limechukua hatua kusaidia wakulima na wafugaji kuepuka madhara makubwa ya majanga ya kiasili kama vile mafuriko ambayo yamekuwa yanakumba mara kwa mara taifa hilo na kusababisha wakulima na wafugaji kupoteza siyo tu mifugo yao bali pia chakula cha mifugo, mazao na makazi yao na hivyo kuwaacha katika lindi la umaskini.

Sauti
2'41"