Vifo vya wahamiaji Mexico; UN yatuma salamu za rambirambi
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ameeleza masikitiko yake kufuatia vifo vya takribani watu 39 katika kituo cha kushikilia wahamiaji nchini Mexico.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ameeleza masikitiko yake kufuatia vifo vya takribani watu 39 katika kituo cha kushikilia wahamiaji nchini Mexico.
Kamishna Mkuu wa haki za binadamu kwenye Umoja wa Mataifa Volker Türk, ameonya kuwa mikakati mipya iliyotangazwa na serikali ya Marekani ya kudhibiti au kulinda mipaka yake inadumaza misinig ya kimataifa ya haki za binadamu.
Shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa maendeleo duniani, UNDP nchini Mexico linafadhili miradi ya maabara za wabunifu wanaopatia majawabu changamoto za kijamii zitokanazo na matatizo yanayowazunguka. Miongoni mwa miradi hiyo ni ule wa kusafisha fukwe za bahari na uchafu unaokusanywa ukiwemo mwani aina ya Sargusssum, kutumika kutengeneza nyumba. Tupate undani wa taarifa hii iliandaliwa na UNDP na kusomwa studio na Evarist Mapesa wa Redio washirika SAUT FM.
Hii leo jaridani tunamulika siku ya kimataifa ya usaidizi wa binadamu duniani ambapo Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa anatoa shukrani kwa wale wote wanaojitolea kuchukua hatua kusaidia wengine hata wenyewe wakiwa bado na shida, huku akikumbuka wale waliopoteza maisha wakisaidia wengine. Tunakwenda pia Mexico huko ambako taka za mwani zinatengeneza matofali. Makala tunabisha hodi Kigoma, Leah Mushi anakuletea simulizi ya wanawake wanufaika wa miradi inayotekelezwa na UNDP chini ya KJP. Mashinani ni wito kutoka kwa Mkuu wa WHO ili kusaidia wakazi wa jimbo la Tigray nchini Ethiopia.
Umoja wa Mataifa hii leo umetoa ripoti yake kuhusu idadi ya watu ambapo idadi ya watu duniani inatarajiwa kuongezeka na kufikia bilioni 8 tarehe 15 mwezi Novemba mwaka huu wa 2022. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres katika ujumbe wake wa siku hii anaweka bayana kuwa ongezeko hilo la idadi ya watu linatokana na sababu kadhaa ikiwemo maendeleo makubwa katika huduma za afya, maendeleo ambayo yamechochea pia kupungua kwa vifo vya wajawazito na watoto wachanga.
Hii leo jaridani tunamulika masuala ya idadi ya watu na amani Sudan Kusini. Katika idadi ya watu ikiwa leo ni siku ya idadi ya watu duniani tunajulishwa kuwa ifikapo tarehe 15 mwezi Novemba mwaka huu idadi ya watu duniani itafikia bilioni 8! Na miongoni mwa nchi ambazo idadi ya watu inaongezeka ni Tanzania na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo. Katika masuala ya amani huko Sudan Kusini mafunzo yameendeshwa ili jamii iweze kuwa sehemu ya kukabiliana na ukatili ikiwemo wa kingono. Makala inakupeleka Mexico kwa msichana ambaye ndoto yake ya kuwa mkunga ili kusaidia jamii yake imetimia.
Kikundi cha wanawake wa Mayan kilichopo katika rasi ya Yucatan nchini Mexico kimeweza kujikwamua kiuchumi baada ya kupata mkopo kutoka Shirika la umoja wa Mataifa la Mpango wa maendeleo UNDP.
Tangu kuanza kwa mwaka 2021 idadi ya watoto wahamiaji wanaowasili Mexico wakisubiri kuingia nchini Marekani imeongezeka kwa kasi kutoka watoto 380 hadi karibu watoto 3500 amesema mkurugenzi wa kanda ya Amerika Kusini na Caribbea wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia Watoto UNICEF.
Mkurugenzi Mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la elimu, sayansi na utamaduni, UNESCO, Audrey Azoulay amelalamikia mauaji ya wanahabari watatu nchini Mexico, ambao ni Edgar Alberto Nava López, Rogelio Barragán Pérez, na Jorge Ruiz Vázquez, akitoa wito kwa mamlaka kuchunguza matendo hayo yaliyofanywa kati ya mwishoni mwa mwezi Julai na tarehe 2 Agosti.
Mexico inatakiwa kufanya uchunguzi wa kina, huru na usioegemea upande kuhusu kutoweka kwa watu mnamo mwaka 2010, kamati ya haki za binadamu imeeleza katika maamuzi yaliyochapishwa leo mjini Geneva Uswisi.