Mbegu za mimea zapandwa nje na ndani ya kituo cha anga za juu
Shirika la Umoja wa Mataifa la nishati ya atomiki, IAEA limesema mbegu za mazao zilizopelekwa kituo cha anga za juu mwezi Novemba mwaka jana tayari zimepandwa eneo la ndani na nje ya kituo hicho na hivyo zinapata miali kamilifu ya anga za juu pamoja na viwango vya juu zaidi vya joto kwenye eneo hilo.