Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Mauritania

Kijana akitembea juu ya mashua karibu na pwani ya Gambia, eneo ambako mamia ya wahamiaji huanza safari zisizo na uhakika kuvuka bahari kila mwaka.
IOM /Lamin Sanneh

IOM yazindua mpango mpya wa kuimarisha uwezo wa Afrika Magharibi kukabiliana na wimbi la wahamiaji wanaopotea

Shirika la Umoja wa Mataifa la Uhamiaji (IOM) leo tarehe 4 mwezi Novemba mwaka 2025, limezindua mpango wa kihistoria kwa kushirikiana na serikali za Gambia na Mauritania, wenye lengo la kuimarisha uwezo wa kitaifa katika kukabiliana na vifo na kupotea kwa wahamiaji wanaosafiri kwenye njia zinazounganisha bara la Afrika na Ulaya.

Mabomu yanayolipuka na kusambaza vilipuzi vingine yanawezakuwa yalitumika Ukraine.
© UNOCHA/Adedeji Ademigbuji

Mabomu yanayolipuka na kusambaza vilipuzi vingine  yameua na kujeruhi mamia ya raia nchini Ukraine tangu mwaka 2022: UNIDIR

Mabomu yanayolipuka na kusambaza vilipuzi vingine  yameua na kujeruhi zaidi ya raia 1,200 nchini Ukraine tangu kuanza kwa uvamizi mkubwa wa Urusi mwezi Februari 2022, kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo na muungano wa mashirika yasiyo ya kiserikali unaoungwa mkono na Taasisi ya Umoja wa Mataifa ya Utafiti wa Udhibiti wa Silaha UNIDIR.

UN News/ Hisae Kawamori

Manusurua kutoka Gambia: Sitamani tena kuzamia kwenda ulaya

Kila mwaka maelfu ya wahamiaji kutoka maeneo mbalimbali ikiwemo Afrika hujaribu kufika Ulaya wakivuka Bahari ya Mediterania wakieleza kwenda kusaka maisha bora lakini safari hiyo inaelezwa kuwa ni hatari sana kwani maelfu ya watu hufa maji au kutoweka. 

Ni Amadou Jobe kijana ambaye akiwa na umri wa miaka 25 alianza safari ya hatari kutoka nchini Kwake Gambia kupitia kaskazini mwa Afrika lengo likiwa Kwenda nchini Italia kusaka maisha bora kwani alikuwa akiishi katika hali ya umasikini na alitamani kuja kuisaidia familia yake iwapo angefanikiwa kufika Ulaya. 

Sauti
3'19"

24 Juni 2022

Hii leo jaridani, Leah Mushi anamulika:
1.    Chuo cha sanaa Kivu, AKA huko Goma jimboni Kivu Kaskazini nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC na harakati za kutumia uchoraji wa kuta ili kuepusha vijana na ghasia sambamba na kulinda mazingira.
2.    Nchini Mauritania IFAD imeleta nuru kwa wakulima waliokosa mvua
3.    Makala tunakwenda Kigali, Rwanda kwenye mkutano wa viongozi wa nchi za Jumuiya ya Madola ambako kijana Paul Siniga kutoka Tanzania amewakilisha vijana.

Sauti
11'49"
Mabadiliko ya tabianchi ni moja ya changamoto zinazoikabili dunia. Ukanda wa Saheli kusini mwa jangwa la Sahara.
© UNDP Mauritania/Freya Morales

Kama sisi tumeweza, wengine washindwe kwa nini? – Wakimbizi Mauritania 

Hivi karibuni, siku chache kabla ya kuanza kwa mkutano wa 26 wa nchi wanachama wa mabadiliko ya tabianchi, #COP26 ambao hivi sasa unaendelea Glascow, Uskochi, Mshauri Maalumu wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudunia wakimbizi, UNHCR kuhusu Hatua dhidi ya Mabadiliko ya Tabianchi, Andrew Harper ametembelea Mauritania kujionea jinsi wakimbizi wanavyopambana na janga la tabianchi.

Sauti
2'5"