Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Mauritania

UN News/ Hisae Kawamori

Manusurua kutoka Gambia: Sitamani tena kuzamia kwenda ulaya

Kila mwaka maelfu ya wahamiaji kutoka maeneo mbalimbali ikiwemo Afrika hujaribu kufika Ulaya wakivuka Bahari ya Mediterania wakieleza kwenda kusaka maisha bora lakini safari hiyo inaelezwa kuwa ni hatari sana kwani maelfu ya watu hufa maji au kutoweka. 

Ni Amadou Jobe kijana ambaye akiwa na umri wa miaka 25 alianza safari ya hatari kutoka nchini Kwake Gambia kupitia kaskazini mwa Afrika lengo likiwa Kwenda nchini Italia kusaka maisha bora kwani alikuwa akiishi katika hali ya umasikini na alitamani kuja kuisaidia familia yake iwapo angefanikiwa kufika Ulaya. 

Sauti
3'19"

24 Juni 2022

Hii leo jaridani, Leah Mushi anamulika:
1.    Chuo cha sanaa Kivu, AKA huko Goma jimboni Kivu Kaskazini nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC na harakati za kutumia uchoraji wa kuta ili kuepusha vijana na ghasia sambamba na kulinda mazingira.
2.    Nchini Mauritania IFAD imeleta nuru kwa wakulima waliokosa mvua
3.    Makala tunakwenda Kigali, Rwanda kwenye mkutano wa viongozi wa nchi za Jumuiya ya Madola ambako kijana Paul Siniga kutoka Tanzania amewakilisha vijana.

Sauti
11'49"
Mabadiliko ya tabianchi ni moja ya changamoto zinazoikabili dunia. Ukanda wa Saheli kusini mwa jangwa la Sahara.
© UNDP Mauritania/Freya Morales

Kama sisi tumeweza, wengine washindwe kwa nini? – Wakimbizi Mauritania 

Hivi karibuni, siku chache kabla ya kuanza kwa mkutano wa 26 wa nchi wanachama wa mabadiliko ya tabianchi, #COP26 ambao hivi sasa unaendelea Glascow, Uskochi, Mshauri Maalumu wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudunia wakimbizi, UNHCR kuhusu Hatua dhidi ya Mabadiliko ya Tabianchi, Andrew Harper ametembelea Mauritania kujionea jinsi wakimbizi wanavyopambana na janga la tabianchi.

Sauti
2'5"

05 FEBRUARI 2020

Katika Jarida la Habari hii leo kutoka Umoja wa Mataifa Anold Kayanda anakuletea
-UNHCR yaongeza hatua za kukabiliana na hali ya wakimbizi Sahel ghasia zikishika kasi
-Somalia inahitaji msaada wa kibinadamu wakati watu milioni 4.1 wakikabiliwa na kutokuwa na uhakika wa chakula
-UNESCO yasema asilimia 32 ya watu wa zaidi ya miaka 15 Nepali hawajui kusoma wala kuandika
-Makala yetu leo inatupeleka mkoani Kagera kumulika mchango wa wauguzi na wakunga
Na Mashinani tuko Afghanistan ambako UNICEF inapambana na utapiamlo

Sauti
11'41"
UNHCR/Federico Scoppa

Watu 58 wafa maji kando mwa pwani ya Mauritania wakielekea Ulaya

Takribani watu 58 wamethibitishwa kufa maji baada ya boti walimokuwa wakisafiria kuzama wakati ikikaribia pwani  ya Mauritania hii leo. Anold Kayanda na maelezo zaidi.

Taarifa ya shirika la uhamiaji la Umoja wa Mataifa, IOM iliyotolewa mjini Nouadhibou hii leo imesema kuwa manusura 83 wanapatiwa msaada kutoka mamlaka za Mauritania, IOM pamoja na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR.

Sauti
1'26"