24 Juni 2022
Hii leo jaridani, Leah Mushi anamulika:
1. Chuo cha sanaa Kivu, AKA huko Goma jimboni Kivu Kaskazini nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC na harakati za kutumia uchoraji wa kuta ili kuepusha vijana na ghasia sambamba na kulinda mazingira.
2. Nchini Mauritania IFAD imeleta nuru kwa wakulima waliokosa mvua
3. Makala tunakwenda Kigali, Rwanda kwenye mkutano wa viongozi wa nchi za Jumuiya ya Madola ambako kijana Paul Siniga kutoka Tanzania amewakilisha vijana.