MachafukoYemen yasababisha misaada kusitishwa: OCHA
Mkuu wa ofisi ya Umoja wa Mataifa ya kuratibu misaada ya kibinadamu OCHA nchini Yemen, Jamie McGoldrick ameomba kusitishwa kwa utoaji wa huduma za kibinadamu nchini humo baada ya mashambulizi ya hivi karibuni yaliyosababisha vifo vya watu 12 na kujeruhi wengi katika mji mkuu Sanaa.
Bwana McGoldrick amesema hali ya usalama kwa watoa huduma wa mashirika tofauti ni hatarishi kutokana na migogoro ya hivi karibuni.